Home BIASHARA Kinachopelekea biashara kufungwa hiki hapa

Kinachopelekea biashara kufungwa hiki hapa

0 comment 22 views

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Godfrey Simbeye amesema biashara nyingi zinafungwa kutokana na uwepo wa mazingira magumu pamoja na sera ambazo kwa kiasi kikubwa zinawakandamiza wafanyabiashara. Simbeye ametoa kauli hiyo mkoani Morogoro katika kongamano la kambi ya ujasiriamali lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Simbeye ameeleza kuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na TPSF, takribani biashara 4,640 zimefungwa ndani ya miaka mitatu kutokana na vikwazo mbalimbali. Ameongeza kuwa TPSF imejipanga kusaidia sekta ya ujasiriamali pamoja na kutoa elimu.

Mbali na hayo, Simbeye ameshauri wanafunzi kuandaliwa na kufundishwa zaidi kuhusu ujasiriamali mapema na kusema kuwa ajira nyingi zaidi zinatokana na sekta hiyo. Amewataka vijana kujiamini na kuondokana na uwoga kwani wao ndio waathirika wakubwa wa tatizo hili.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter