• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Ubunifu wa mavazi umekomboa wengi

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in BIASHARA, UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Katika harakati za kupiga vita umaskini, kundi kubwa la watu hasa vijana wamekuwa wakiwekeza katika ubunifu wao ili kuja na vitu tofauti ambavyo vitawaingizia kipato. Ikilinganishwa na miaka ya nyuma, vijana wengi zaidi wamekuwa wakijiingiza katika masuala ya ubunifu wa mavazi. Biashara hii imejipatia umaarufu mkubwa miaka ya hivi karibuni. Mojawapo ya sababu ya hilo ni wabunifu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii hasa Instagram kutangaza kazi zao hivyo kuwafikia wateja wengi zaidi ndani na hata nje ya nchi.

Awali, fani hii ilionekana kuwafaa vijana wa jinsia ya kike tu japokuwa kuna wabunifu wa kiume ambao wamefanya vizuri na wamefanikiwa kama vile Mustafa Hassanali na Ally Rehmtullah. Lakini kadri miaka inavyozidi kwenda, dhana hiyo imepoteza nguvu na tumeweza kushuhudia vijana wa kiume wakijikita katika ubunifu na kazi zao kupokelewa vizuri. Mabadiliko haya yanaashiria kuwa haijalishi jinsia yako, kama una kipaji na malengo, unaweza kufika mbali.

Ubunifu wa mavazi umekuwa suluhisho hata kwa vijana ambao wamehitimu masomo yao. Wengi wameona badala ya kuhangaika na kupoteza muda kusaka ajira, ni bora wawekeza kile kidogo walichonacho katika biashara hii kwani mavazi ni mojawapo ya mahitaji ya msingi kwa kila binadamu hivyo soko la biashara hii ni ya uhakika. Kinachotakiwa katika hili ni kuangalia wale unaowalenga na kufanya huduma yako kuwa rafiki ili bidhaa zako zipate soko kwa urahisi.

ADVERTISEMENT

Vilevile, mbunifu wa mavazi anapaswa kwenda na wakati. Anatakiwa kufahamu kinachoendelea katika ulimwengu wa mitindo ili asipitwe. Kazi hii inahitaji umakini wa hali ya juu kwani unatakiwa kusikiliza kile mteja anachohitaji na kuhakikisha kuwa anaridhika na huduma anayopatiwa. Biashara hii kadri siku zinavyokwenda inakumbwa na ushindani katika soko lakini kinachowatofautisha wabunifu hawa ni vipaji vyao, gharama za huduma wanayotoa na namna wanavyojitangaza ili kuwafikia watu wengi zaidi.

Mitandao ya kijamii ina mchango mkubwa katika maendeleo kama ikitumika vizuri. Wabunifu wachanga wamekuwa wakitangaza biashara zao kwa urahisi na hivyo imerahisisha wao kuwafikia watu zaidi. Mitandao ya kijamii pia imekuwa inatumika kama kioo cha kuangalia kile wengine wanafanya na kujifunza, kuomba ushauri, kupata maarifa ili kuboresha biashara husika na kufanya kitu ambacho kitavutia idadi kubwa ya watu.

Tags: biasharaInstagramUbunifu wa mavazi
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Bilioni 17 kutumika katika upanuzi wa uwanja wa ndege wa Karume

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In