• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Saturday, June 25, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Mitandao ya kijamii inavyoweza kuharibu bajeti yako

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in FEDHA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Katika miaka ya hivi karibuni kundi kubwa la watu hasa vijana wamekuwa wakitumia mitandao kama vile Facebook na Instagram kama mahali pa kuonyesha biashara, ubunifu na vipaji vyao kwa lengo la kujitangaza ili kupata wateja. Mitandao hii imesaidia kwa kiasi kikubwa kwani imekuwa njia rahisi ya kujiingizia kipato. Lakini kwa upande wa pili, kuna kundi la watu ambao hujikuta wanatumia pesa zaidi kufanya manunuzi mtandaoni na hali hiyo inapelekea wao kuwa na matumizi mabaya ya fedha.

Ifahamike kuwa, wafanyabiashara wa mitandaoni wapo kwa dhumuni moja tu ambalo ni kutengeneza pesa. Wakati mwingine wanafanya kazi na wasanii au watu maarufu ambao ushawishi wao ni mkubwa katika jamiii ili kuwavuta zaidi wateja wao ili mradi tu wauze bidhaa zao. Watu wengine hushindwa kujizuia na kujikuta wakiingia gharama kubwa kununua bidhaa wanazoziona mtandaoni wakiamini kuwa wasipokuwa na bidhaa hiyo wanapitwa ama wanaonekana kama watu ambao hawaendi na wakati.

ADVERTISEMENT

Ushawishi kutoka kwa marafiki pia inachangia kwa kiasi kikubwa katika hili. Vijana ndio waathirika wakubwa wa kufanya maamuzi yasiyo ya busara kifedha kutokana na ushawishi. Unajikuta unashawishika kununua vitu fulani mitandaoni au kwenda mahali fulani ambapo kwa mujibu wa mitandao ya kijamii ndio sehemu ya kijanja na bila kuangalia bajeti yako unatumia fedha nyingi kuliko kawaida. Vitendo kama hivi vinarudisha nyuma watu wengi na wanajikuta wanashindwa kutimiza malengo muhimu zaidi waliyonayo.

Mtu anayetumia muda mwingi katika mitandao ya kijamii kwa namna moja au nyingine hujikuta akitamani vitu au huduma fulani mara baada ya kuona kwa watu wengine. Hali hiyo ni ya kibinadamu na mara nyingi huwezi kuiepuka. Hii inakuja kama athari mojawapo ya kutumia mitandao kwa muda mrefu. Ni lazima kubadilika na kujifunza kutumia busara zaidi katika masuala haya kwani wafanyabiashara mitandaoni ni wengi na huwezi kuwamaliza wote. Tumia mitandao katika njia ambayo haitakusababishia hasara na kuharibu bajeti yako. Ni kweli kuwa kufanya manunuzi mtandaoni ni rahisi kwani unatumia muda mfupi kupata huduma lakini umakini unatakiwa ili kuhakikisha kuwa matumizi yako yanaendana na bajeti yako.

Mitandao ya kijamii ikitumika kistaarabu, inakuwa jukwaa zuri la kujifunza, kuwasiliana na kushauriana na watu mbalimbali, kupata elimu ya ujasiriamali na kujitangaza kwa watu. Kama jamii, ni vizuri tukatambua mchango mkubwa wa teknolojia katika maendeleo. Vijana wengi wameweza kutumia jukwaa la mitandao kujiingizia kipato hivyo uhamasishaji zaidi uendelee kutolewa ili kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya biashara na huduma mbalimbali. Wanunuzi nao wanatakiwa kuwa makini ili wasijikute wanatumia fedha kupita kiasi sababu ya biashara za mitandaoni.

Tags: bajetibiasharaMitandao ya kijamii
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Wanawake washirikishwe zaidi kiuchumi- Balozi Donnell

Soko la ajira nchini liwapatie fursa zaidi wanawake

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In