• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Friday, March 31, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Sherehe zisikuache maskini

Patricia Richard by Patricia Richard
June 27, 2018
in FEDHA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Imekuwa ni desturi yetu hapa nchini kwa watu kutumia gharama kubwa katika sherehe mbalimbali. Wahusika hutafuta huku na kule mpaka kuhakikisha kuwa yale yote yaliyolengwa yanafanikiwa. Ni jambo la heri kusherekea, hilo halina pingamizi lakini kwanini tunaenda nje ya uwezo wetu ili tu kutumia fedha zote hizo ndani ya siku moja? Haiwezekani kwa watu kufanya sherehe kwa kuangalia uwezo walionao? Kuna ulazima wa kuingia gharama kubwa ili tu kusherekea? Je, maisha baada ya sherehe yanakuwa vipi?

Ukweli ni kwamba kila mtu anatamani kufanya sherehe nzuri. Kila mmoja wetu anatamani kufanya vitu vikubwa katika siku hiyo muhimu lakini tunajipanga kiasi gani kupambana na hali ya maisha baada ya hapo? Kwanini kiasi fulani cha fedha hizo zisiwekezwe katika maisha ya baadae? Katika elimu? Kwa watoto na vitu vingine ambavyo bila shaka vina umuhimu mkubwa zaidi?

Sherehe na hafla mbalimbali sio kitu kibaya. Ni vizuri kukaa pamoja, kujumuika na kusherekea mafanikio mbalimbali tunayopata katika maisha. Tatizo ni pale ambapo gharama kubwa inatumika wakati inawezekana kabisa kufanya sherehe iliyo ndani ya uwezo wako kiuchumi. Fedha nyingine zingeweza kuelekezwa katika masuala ya kimsingi na kimaendeleo badala ya muziki, chakula na vinywaji pekee. Jamii yetu inapaswa kuangalia suala hili katika mtazamo tofauti na kujenga desturi ya kuwasaidia wapendwa wao kusonga mbele kimaisha mbali ya kuwafanyia sherehe za kifahari. Bila shaka hiyo itakuwa zawadi nzuri na yenye manufaa.

ADVERTISEMENT

Itakuwa vizuri kama tukibadili mitazamo yetu katika masuala ya sherehe. Ni wakati wa kutumia fedha zinazopatikana kwa ustaarabu na busara. Hakuna umuhimu wa kufanya sherehe ya gharama wakati ungeweza kutumia kiasi fulani cha fedha hizo kujiendeleza. Bajeti zetu ziendane na hali yetu ya maisha ili kuruhusu watu waweze kuwa katika nafasi nzuri kiuchumi hata baada ya sherehe hizi kukamilika. Muda umefika sasa wa kubadilisha dhana ya kwamba ili sherehe iwe sherehe nzuri basi lazima gharama kubwa itumike. Badala yake, tujifunze kupangilia sherehe, tuwe makini katika bajeti na la muhimu zaidi, tufahamu kuwa kuna maisha baada ya sherehe.

Jambo la msingi kufanikisha sherehe ni uwepo wa ndugu, familia, marafiki na majirani kwani maana halisi ya sherehe ni kufurahia kwa pamoja  na wale unaowathamini. Kuna kila sababu ya kufanya sherehe kwa kuangalia uwezo ulionao. Gharama ya maisha zinaendelea kupanda kadri miaka inavyokwenda hivyo basi hamna haja ya kuingia gharama kubwa na kujirudisha nyuma kimaendeleo eti kwa sababu tu ni sherehe. Yapo mambo ya msingi zaidi ya kufanya katika maisha hivyo kuwa makini na maamuzi yako kwani yanaweza kukuletea madhara siku za mbele.

Tags: fedhaGharamaSherehe
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Mnangagwa kutua nchini leo

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda.

10m kwa mshindi wa Tuzo ya Taifa ya Mwl Nyerere

March 31, 2023

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda.

10m kwa mshindi wa Tuzo ya Taifa ya Mwl Nyerere

by Pesatu Reporter
March 31, 2023
0

Kilele cha Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu kinatarajia kufanyika Aprili 13, 2023 Jijini Dar es Salaam...

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In