• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Tuesday, October 3, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Trilioni 7.37 zakusanywa na serikali ndani ya miezi mitano

Serikali imekusanya makusanyo ya ndani ya Sh. 7.37 trilioni, sawa na asilimia 88.9 ya makadirio ya Sh. 8.30 trilioni katika kipindi hicho.

Patricia Richard by Patricia Richard
December 31, 2018
in FEDHA
0
Tanzania yaridhia mtaji AfDB kuongezwa

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango.

Share on FacebookShare on Twitter

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango amesema katika kipindi cha miezi mitano ya kwanza yaani Julai hadi Novemba 2018, serikali imekusanya makusanyo ya ndani ya Sh. 7.37 trilioni ambayo ni sawa na asilimia 88.9 ya makadirio ya Sh. 8.30 trilioni katika kipindi hicho. Waziri Mpango amesema hayo jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya hali ya uchumi wa taifa na utekelezaji wa bajeti ya serikali.

Katika maelezo yake, Waziri huyo amesema katika kipindi hicho, mapato ya kodi yalifikia Sh. 6.23 trilioni ikiwa ni sawa na asilimia 88 ya lengo la kukusanya Sh. 7.04 trilioni kwa kipindi hicho. Vilevile, mapato yasiyo ya kodi yalifikia Sh. 936.03 bilioni sawa na asilimia 21 zaidi ya lengo la Sh. 775.36 bilioni huku mapato ya halmashauri yakifikia Sh. 203.8 bilioni, sawa na asilimia 61 ya lengo.

ADVERTISEMENT

Mbali na hayo, Dk. Mpango ameeleza kuwa ongezeko la mapato yasiyo ya kodi limetokana na kuimarishwa kwa ufuatiliaji kwenye taasisi, mashirika na kampuni kulikopelekea serikali kupata michango na gawio stahiki kutoka kwenye uwekezaji wake. Aidha, kuimarika kwa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji wa maduhuli kwenye wizara na idara zinazojitegemea kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Mapato (GePG) ambapo kati ya Julai 2017 hadi Novemba 2018, takribani taasisi za serikali 325 zimetumia mfumo huo kukusanya maduhuli.

Kuhusu jitihada za kuboresha mazingira ya kufanya biashara, Dk. Mpango amesema serikali kupitia Sheria ya Fedha 2018/19 ilipunguza baadhi ya ada na tozo ambazo zilikuwa kero kwa wananchi zikiwemo za mazingira, TBS, TFDA na tozo kwenye madini ya chumvi. Kuhusu changamoto ya ukusanyaji mapato, Waziri huyo amesema hali hiyo inatokana na ukwepaji wa kodi, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu umuhimu wa kudai risiti pale wanapofanya manunuzi na wafanyabiashara kutoa risiti pale wanapofanya mauzo pamoja na wigo mdogo wa kodi.

Tags: biasharaDk. Philip MpangoDodomaGePGkodimapato
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Matajiri wanatumiaje pesa zao?

Deni la taifa laongezeka

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Exim kulinda maslahi watumiaji huduma za bima

September 26, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Exim kulinda maslahi watumiaji huduma za bima

by Pesatu Reporter
September 26, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In