Home VIWANDAMIUNDOMBINU Serikali yazidi kuwekeza katika miradi ya maji

Serikali yazidi kuwekeza katika miradi ya maji

0 comment 26 views

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Prof. Makame Mbarawa amesema hadi Juni 2020, miradi ya maji takribani 1,801 itakuwa imetekelezwa ambapo hadi kufikia sasa, miradi 500 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Prof. Mbarawa amesema hayo wakati wa kuweka jiwe la msingi katika mradi wa majisafi na majitaka jijini Arusha ambapo ameeleza kuwa miradi hiyo imeelekezwa katika maeneo mbalimbali yanayokumbwa na tatizo la maji ili kuhakikisha kuwa lengo la serikali la kuwapatia wananchi majisafi linatimia.

“Miradi hii inatuhakikishia kuwa ifikapo 2020 kupitia ilani ya CCM ambayo inasema watu wote wanaoishi katika mikoa wapate maji kwa asilimia 95, wilaya asilimia 90 na vijiji asilimia 85”. Amesema Waziri Mbarawa.

Mradi huo uliozinduliwa jijini Arusha wenye thamani ya Sh. 520 bilioni ni moja kati ya miradi inayotekelezwa hivi sasa ambapo Waziri huyo amewahakikishia wananchi kuwa, maji yatapatikana muda wote.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter