• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, September 24, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

TAA kuboresha huduma zake

"Kuanzia Januari mwaka inapoanza tutajitahidi kufanya kazi kwa weledi na kwa uadilifu mkubwa"

Patricia Richard by Patricia Richard
December 20, 2018
in MIUNDOMBINU
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Richard Mayongela akimueleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (kulia), changamoto zinazoikabili Mamlaka hiyo, wakati alipotembelea kukagua miundombinu mbalimbali kwenye kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Richard Mayongela akimueleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (kulia), changamoto zinazoikabili Mamlaka hiyo, wakati alipotembelea kukagua miundombinu mbalimbali kwenye kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Share on FacebookShare on Twitter

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Richard Mayongela, amesema wamejipanga kufanya maboresho makubwa katika miundombinu ya viwanja vya ndege nchini pamoja na katika kuhamasisha kasi ya utendaji ya wafanyakazi katika mamlaka hiyo. Mayongela ametoa ahadi hiyo mbele ya Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe katika mkutano na waandishi wa habari baada ya kufanya ukaguzi wa miundombinu katika jengo la abiria la kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

“Kwa niaba ya wenzangu tunakuahidi kwamba kuanzia Januari mwaka inapoanza tutajitahidi kufanya kazi kwa weledi na kwa uadilifu mkubwa. Kwa upande wa kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere kuendelea kulalamikiwa kwa mambo madogo madogo ya kiutendaji haipendezi na ni aibu kwetu, mimi mwenyewe kama Mtendaji Mkuu nitachukua hatua na kuhakikisha kwamba tunakipa hiki kiwanja kipaumbele”.

ADVERTISEMENT

Waziri Kamwelwe alianzia ziara yake katika kiwanja cha ndege cha Songwe na kugundua kuwa njia ya kuruka na kutua ndege imejengwa chini ya kiwango na mkandarasi. Baada ya kutua JNIA, alibaini pia baadhi ya changamoto na kutoa maagizo kwa TAA kufanya mabadiliko ya kiutendaji kuanzia Januari mwakani.

“Nawaomba ndugu zangu kuanzia Januari mwakani mbadilike na kama mtu hatabadilika basi tutamtoa. malalamiko ya watu mimi nayapokea na ninayafanyia kazi, kwa maana hiyo ni vyema pia myafanyie kazi”. Amesema Mhandisi Kamwelwe.

Tags: Isack KamwelweJNIASongweTAA
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
COSTECH yafadhili utafiti Dodoma

Mavunde: Zabibu utambulisho wa Dodoma

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In