• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Watanzania watakiwa kuchangamkia udhamini wa UNESCO

Athanas Lupatu by Athanas Lupatu
June 24, 2019
in WANAWAKE NA MAENDELEO
0
Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja Kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo (kushoto), Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto (wa pili kushoto),Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia), pamoja na na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo (kulia) katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja Kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo (kushoto), Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto (wa pili kushoto),Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia), pamoja na na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo (kulia) katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Share on FacebookShare on Twitter

Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo amewataka Watanzania kuchangamkia ufadhili wa masomo unaotolewa na shirika hilo ili kutanua uwezo wa rasilimali watu katika nyanja mbalimbali.

Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-UNESCO), Profesa Hamisi Malebo akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi. Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati wa kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kwa Mtanzania, Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship .

Mtanzania huyo kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania atakwenda Japan na Canada kwa miezi minne kufanikisha utafiti wake juu ya menejimenti ya ufahamu wa data katika Tehama unavyoweza kusaidia mfumo wa kujifunza wa wanafunzi.

Doreen ameibuka mshindi kati ya watu 280 walioomba nafasi hiyo.

Bi. Doreen Richard Mushi kutoka Chuo Kikuu Huria (OUT) akizungumza jambo mara baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Profesa Malebo aliwataka watanzania kutumia nafasi mbalimbali zinazotangazwa kushindaniwa na taasisi yake kutafuta masomo na kwamba taasisi hiyo huchagua kwa haki kwa kuzingatia vigezo na ushindani uliopo.

ADVERTISEMENT

Alisema kwa sasa watu wengi hawajitokezi kuomba nafasi hizo za ufadhili kupitia Unesco, na kuwataka waombe kwa kuwa nafasi hizo huenda yule anayestahili kwenda kutokana na vigezo vilivyopo ambavyo ni vya kishindani.

“Natoa wito kwa watanzania kutumia nafasi tunazopewa na Unesco kwani ni msaada mkubwa katika kuimarisha na kuboresha elimu na kuwezesha watanzania hasa vijana kupata elimu ya kusaidia kusogeza mbele maisha” alisema Profesa Malabo.

Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako ameishukuru serikali ya Japan kwa kuwezesha Unesco kutoa ufadhili huo muhimu kwa taifa hili.

Akimwakilisha Waziri Ndalichako, Naibu Makamu Mkuu  wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Prof Cuthbert Kimambo  alisema kwamba serikali ya Tanzania pamoja na kushukuru Japan kwa kumwezesha Mtanzania huyo, pia inaamini wale waliomaliza mafunzo yao watarejea nchini na kuyafanyia kazi yale waliojifunza na kuleta maendeleo.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati wa hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi. Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Alisema pamoja na kuleta ufanisi katika ubadilishanaji wa maarifa kupitia mafunzo hayo ni matarajio ya serikali kwamba wanaopewa mafunzo hayo watahamisha elimu hiyo kwa wenzao na kulisogeza mbele zaidi gurudumu la maendeleo.

Mpango wa masomo wa kutanua uwezo wa utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship ulianzishwa mwaka 2000 na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Unesco Koichiro Matsura kwa kutafakari maono ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan wakati huo , Keizo Obuchi ambaye aliamini katika uwezo wa watu katika kuibadili na kuijenga dunia hivyo haja ya kujiongezea maarifa zaidi ili kuwepo na maendeleo.

Lengo la programu hiyo ni kuwezesha kuwa na uhakika katika utunzaji wa mazingira, kuleta mazungumzo ya kimataifa na kuendeleza suala la mawasiliano na teknolojia. Programu hii ni matokeo ya ushirikiano kati ya serikali ya Japan na UNESCO katika kuendeleza rasilimali watu kwa nchi zinazoendelea.

Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto akimpongeza Bi. Doreen Richard Mushi kutoka Chuo Kikuu Huria (OUT) kwa kushinda tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Programu hii ambayo ilianzishwa mwaka 2001, imeshawezesha watu 290 hasa vijana watafiti, ambapo 82 wametoka Afrika, kutanua uwezo wao katika nyanja wanazozifanyia kazi.

Miongoni mwa nchi ambazo zimeshanufaika ni Tanzania ambapo katika programu ya mwaka 2014 na 2015, Fatuma Ubwa na Juliana Samuel Kamaghe, walipata nafasi ya kujiimarisha katika sekta ya habari na teknolojia ya mawasiliano.

Doreen Richard Mushi ambaye amekuwa mshindi wa UNESCO/Keizo Obuchi Research Fellowships ya mwaka 2018 alikuwa anashindana na watu wengine 280 na ameshinda katika nyanja ya habari na teknolojia ya mawasiliano (Tehama).

Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The UNESCO/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa na maafisa wa Ubalozi wa Japan katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan jijini Dar es Salaam.

Tuzo hiyo itamwezesha Doreen Mushi kufanya kazi kwa miezi miwili na watafiti wa taasisi ya Learning Analytics Centre ya Chuo Kikuu cha Kyushu nchini Japan, na miezi mingine miwili na watafiti wa kitivo cha elimu, Chuo Kikuu cha British Columbia mjini Vancouver, Canada.

Katika vyuo vyote viwili  Doreen Richard Mushi, aliyezaliwa Agosti 27, 1983 atafanya utafiti kuhusu takwimu na uchambuzi utakaosaidia mifumo ya kusoma kwa wanafunzi.

Tags: Doreen MushiProf. Joyce NdalichakoUNESCO
Athanas Lupatu

Athanas Lupatu

Next Post
Punguza gharama kwa kufanya haya

Taasisi za fedha mkombozi wa wajasiriamali

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In