• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, February 5, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Benki zifanye hivi kuwateka vijana

Vijana hufurahia zaidi watoa huduma wanaowaelewa na kuwasiliana nao kwa ukaribu.

Abdul Kassim by Abdul Kassim
June 22, 2020
in BENKI, BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Utandawazi na uvumbuzi wa teknolojia za kisasa vimeendelea kuchangamsha taasisi za fedha hususani benki kwenda na wakati ili kutimiza mahitaji ya wateja wao. Vijana ni sehemu ya wateja ambao benki zinatakiwa kuwahamasisha zaidi kuendelea kutumia huduma kwa ajili ya masuala mbalimbali ya kifedha kwa sababu hawataki kufanyiwa maamuzi ya kifedha bali wanataka kufanya maamuzi yao wenyewe, wanataka kupata taarifa kwa urahisi zaidi kupitia mtandao bila kwenda benki moja kwa moja.

Inaelezwa kuwa asilimia 34 ya vijana hawafurahishwi na hali yao ya kifedha huku asilimia 60 wakielemewa na madeni. Taasisi za kibenki zinaweza kutumia nafasi hiyo kuwafikia vijana lakini kwa namna ambayo itawafanya watilie mkazo na si kupuuzia matangazo yanayohusu huduma za benki kama ambavyo wamekuwa wakifanya.

Vijana wanataka huduma kwa uharaka, urahisi na uwezo wa kujihudumia. Vilevile wanapendelea zaidi huduma ambayo inapatikana saa na mahali popote hivyo benki zinatakiwa kuhakikisha huduma zao zinapatikana kwa urahisi, katika vifaa vya kisasa vya kielektroniki. Kwa mfano CRDB kupitia huduma ya Sim Banking hupendelea kutuma ujumbe kwa wateja wao kuhusu huduma wanazozitoa. Hili ni jambo zuri na linaweza kuwa limewahamasisha vijana wengi. Ni muhimu kwa benki kufanya utafiti kila wakati ili kwenda na wakati na kuhakikisha kuwa wanapata mrejesho mzuri.

ADVERTISEMENT

Benki zinatakiwa kutambua kuwa vijana sio waoga wa hatari, au teknolojia zinazoendelea kuundwa bali wao ni waoga wa kutopata vitu wanavyotaka ndani ya muda na kwa urahisi. Hivyo benki zinashauriwa kuwekeza katika teknolojia za kisasa zaidi ili kuhakikisha huduma zinawafikia vijana kwa urahisi zaidi, kwani idadi ya vijana ni kubwa sana hivyo kwa kuwafikia kwa urahisi mamilioni ya vijana kutanufaisha zaidi benki.

Kwa vijana, suala la kumbukumbu ni muhimu zaidi kuliko kitu kingine na ndio maana utaona kila siku mamia ya vijana wanatuma picha au video mbalimbali katika mitandao ya kijamii kuhusu uzoefu waliopata katika tukio fulani au kwa kwenda mahali fulani. Benki zichukue fursa kama hizo kuwavutia vijana kwa mfano hivi karibuni Wasafi Festival inaanza na hili ni tamasha linalopendwa zaidi na vijana hivyo benki yoyote inaweza kuwahamasisha vijana kufungua akaunti katika benki husika, ambapo baada ya kufungua watu 10 au 50 watapata zawadi ya tiketi ya tamasha hilo, vijana hata ,1000 wanaweza kufungua akaunti katika benki hiyo ili waweze kujipatia tiketi. Na kupitia mambo kama hayo kutaleta muamko kwa vijana kuhusu benki husika na mambo mazuri wanayoweza kuyapata katika benki hiyo.

Ili kuhamasisha vijana, benki zinatakiwa kujihusisha na vijana kwa ukaribu zaidi kwani vijana hufurahishwa zaidi na watoa huduma ambao wanawaelewa. Pia kwa kuweka huduma zao kwa mfano kutangaza huduma za elimu ya fedha, mikopo, uwekaji wa akiba n.k katika mtazamo ambao utawagusa vijana kutumia huduma za benki.

Watu maarufu na wenye ushawishi ni moja ya njia ya kuwahamasisha vijana kutumia huduma za benki. Standard Chartered ilizindua mfumo mpya ambao unawawezesha wateja wake kupata huduma zaidi ya 70 za kujihudumia na kumtangaza msanii maarufu wa muziki hapa nchini Vanessa Mdee kama mwakilishi wa huduma hiyo katika promosheni mbalimbali.

Bado sekta ya benki ina kazi kubwa ya kuwahamasisha vijana watumie huduma zao lakini kwa kutumia mbinu sahihi, taasisi hizi zina uhakika wa kuwa na mahusiano mazuri na vijana kwa sasa na siku zijazo.

Abdul Kassim

Abdul Kassim

Next Post

SERIKALI YAJENGA MAABARA YA KISASA MKOANI KILIMANJARO

Discussion about this post

Habari Mpya

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

January 31, 2023
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

January 31, 2023
Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amewataka vijana nchini Tanzania kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo kupitia utekelezaji wa...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amesema kipindi cha mwezi July...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In