• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Uharibifu katika fukwe za bahari Zanzibar wahatarisha utalii

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Zanzibar ni moja kati ya visiwa maarufu kabisa hapa Afrika. Kwa mujibu wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, wageni zaidi ya 300,000 hutembelea visiwa hivyo kila mwaka. Watalii hupendelea vivutio mbalimbali vilivyopo kisiwani humo. Kwa kiasi kikubwa uchumi wa Zanzibar unategemea sana tabia nchi kwani shughuli za utalii huangalia kwa kiasi kikubwa hali ya hewa. Uchumi wa visiwa hivi pamoja na maisha ya wananchi wake kwa ujumla hutegemea sana hali ya hewa kwani wamezungukwa na maji.

Watalii wengi hupenda kutembelea visiwa hivyo kujionea vivutio kama fukwe mbalimbali za bahari pamoja na maeneo mengine ya kihistoria. Sekta ya utalii ndiyo chanzo kikubwa cha mapato kwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar lakini miaka ya hivi karibuni baadhi ya wananchi wamekuwa wakiendesha shughuli hatarishi ufukweni mwa bahari hali ambayo inatishia kasi ya utalii mahali hapo.

ADVERTISEMENT

Fukwe ni miongoni mwa  vivutio vinavyopendwa zaidi na wageni wanaotembelea Zanzibar  lakini ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya wananchi wanaoishi karibu na bahari  wakizitumia vibaya fukwe hizo kwa kuzifanyia uharibifu na kusababisha fukwe zile kuharibika na kupoteza ubora wake, hali ambayo kama ikiendelea inaweza kuathiri sekta nzima ya utalii ambayo mbali na kuingizia serikali mapato, pia ni chanzo kikubwa cha ajira kwa wazanzibari walio wengi.

Baada ya serikali kutoa agizo la kuwataka wananchi kuacha shughuli za uchimbaji mchanga ndipo changamoto hii ilipoanza kujitokeza kwani wananchi hao walianza kufanya shughuli hizo katika fukwe za bahari. Kuendelea kwa shughuli hizi mbali na kuondoa haiba pia kunaweka dosari katika upatikanaji wa mapato kupitia utalii kwani hakuna mtalii atakayefurahishwa na kuitangaza vizuri Zanzibar huko nje ikiwa wananchi wake wanaendelea kuharibu vivutio hivyo na kuikosesha serikali mapato.

Serikali kuanzia ngazi ya chini kabisa wanapaswa kuwaelimisha wananchi juu ya madhara makubwa ambayo shughuli hizi za uchimbaji zinaweza kuleta visiwani hapo. Pia wanayo nafasi kubwa ya kuzisimamia na kuzifanyia ulinzi kwa umakini mkubwa fukwe ili kuzinusuru na uharibifu huo unaoendelea. Vilevile, sheria kali ziwekwe ili kuwaadhibu wale wote watakaokamatwa kwa makosa haya.

Tags: mapatouchumiutaliizanzibar
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Benki kuu kuunganisha Twiga Bancorp na TPB

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In