• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, February 5, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Tutafanikisha Tanzania ya viwanda bila kilimo cha uhakika?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in VIWANDA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Ili kufanya kazi, viwanda vinahitaji malighafi za kutosha kuzalisha bidhaa ambazo baadae zitatumika kwa matumizi mbalimbali. Serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa ni nchi itakayojijenga kiuchumi kupitia viwanda, jambo ambalo limepokelewa kwa mikono miwili na wadau wa maendeleo. Lakini tupo tayari kwa ajili ya hatua hiyo? Tuna malighafi ya uhakika? Sekta ya kilimo imejipangaje kufanikisha uchumi wa viwanda?

Lazima tukubali kuwa ili viwanda viwepo, lazima sekta ya kilimo iimarike. Lazima wakulima wetu wapatiwe elimu zaidi kuhusiana na kilimo bora na cha kisasa kwani walio wengi bado wanafanya kilimo cha kubahatisha. Lazima wakulima waachane na kilimo cha kutegemea mvua. Ili kufanikisha azma ya serikali ni lazima kuelekeza maofisa kilimo zaidi vijijini ili kuhakikisha kuwa wakulima kote nchini wanafikiwa na kupatiwa fursa za kukuza kilimo chao.

ADVERTISEMENT

Viwanda haviwezi kuzalisha pasipo kuwa na malighafi ambayo inatokana na kilimo. Uwekezaji zaidi unatakiwa katika sekta hii ili kutengeneza mazingira bora zaidi ya uchumi wa viwanda. Sekta ya kilimo ikifanikiw kusimama imara basi viwanda navyo havitayumba kwani kutakuwepo na malighafi ya kutosha hivyo uzalishaji utaendelea bila matatizo. Unaweza kusema kuwa sekta hizi mbili ni kama mapacha. Zinahitaji kufanya kazi kwa pamoja. Hiyo basi kwanini tusielekeze nguvu zaidi kuboresha kilimo chetu?

Huu ni wakati muafaka wa kuwaelimisha wakulima kuhusu kilimo cha umwagiliaji, kilimo biashara, kufanya kilimo chao kwa kutumia teknolojia za kisasa na vilevile kuwapa kipaumbele katika masuala ya mikopo ili kuwezesha kasi ya kilimo kwenda sambamba na ile ya viwanda kwani kufanya hivyo kutawapa uhakika wa soko wakulima na vilevile kutawezesha viwanda kutekeleza majukumu ya uzalishaji pasipo tatizo lolote.

Kilimo ni sekta ambayo inaajiri watanzania wengi na inakadiriwa kuchangia takribani 23% ya pato la taifa ikiunganishwa na uvuvi na ufugaji. Hivyo basi changamoto zilizopo zikiendelea kutafutiwa suluhu, watu wengi zaidi wanaweza kupata ajira kupitia sekta hii na uwepo wa wakulima wengi zaidi unahakikishia uwepo wa viwanda vya kudumu hapa nchini ambavyo navyo vitazalisha ajira kwa kiasi kikubwa.

Sera hii ya uchumi wa viwanda itafanikiwa kwa asilimia mia moja endapo mapinduzi makubwa yatafanyika kuimarisha kilimo hapa nchini. Viwanda vinahitaji malighafi na malighafi hizo ni matokeo ya kilimo bora. Wakulima waelimishwe na watengenezewe mazingira ya kufanya kilimo cha kisasa ambacho kinatumia teknolojia kama ambavyo nchi zienye mafanikio katika kilimo zinafanya. Tukifanikiwa katika hili, basi bila shaka Tanzania ya viwanda nayo itawezekana.

Tags: ajirakilimoTeknolojiauchumiuwekezajiviwanda
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Uharibifu katika fukwe za bahari Zanzibar wahatarisha utalii

Discussion about this post

Habari Mpya

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

January 31, 2023
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

January 31, 2023
Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amewataka vijana nchini Tanzania kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo kupitia utekelezaji wa...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amesema kipindi cha mwezi July...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In