• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Libya yavutiwa na sera za uwekezaji nchini

Patricia Richard by Patricia Richard
October 18, 2018
in UWEKEZAJI
0
Kaimu Rais wa Chama cha Wafanyabiashara,wenye viwanda na Kilimo TCCIA Bw.Octavian Mshiu akisalimiana na Kaimu Balozi wa Libya Nchini Tanzania Bw.Saleh Kusa Arze kwenye Makao Makuu ya TCCIA yaliyopo Posta Jijini Dar es salaam mara baada ya Kaimu Balozi huyo kutembelea ofisini hapo na kujadiliana masuala ya kibiashara.

Kaimu Rais wa Chama cha Wafanyabiashara,wenye viwanda na Kilimo TCCIA Bw.Octavian Mshiu akisalimiana na Kaimu Balozi wa Libya Nchini Tanzania Bw.Saleh Kusa Arze kwenye Makao Makuu ya TCCIA yaliyopo Posta Jijini Dar es salaam mara baada ya Kaimu Balozi huyo kutembelea ofisini hapo na kujadiliana masuala ya kibiashara.

Share on FacebookShare on Twitter

Na Grace Semfuko-MAELEZO

Sera nzuri za uwekezaji zinazotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, zimeanza kuzaa matunda ambapo Serikali ya Libya inaangalia uwezekano wa kuja kuwekeza katika sekta ya Nishati ya umeme.

Kaimu Balozi wa Libya hapa Nchini Saleh Kusa Arze, amesema tayari wameziona fursa za uwekezaji na hivyo wameanza mchakato wa kuja kuwekeza  na tayari kampuni moja ya Nchini Libya imeonyesha nia ya kuwekeza kwenye umeme wa maji au gesi asilia wa megawatt 400.

Hayo yamebainishwa na Balozi Arze katika mazungumzo yake na Chama cha Wafanyabishara wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) alipotembelea kwenye ofisi hizo ili kuangalia fursa za kibiashara na uwekezaji baina ya Libya na Tanzania.

Katika mazungumzo hayo nchi ya Libya mbali na kuonyesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya umeme pia wamesema wameona kuna fursa kubwa kwenye kilimo na kwamba wanaangalia uwezekano wa kuhamasisha wawekezaji wengi zaidi kutoka Libya.

ADVERTISEMENT

Naye Kaimu Rais wa TCCIA Octavian Mshiu amesema ujio wa balozi huyo umekuwa wa mafanikio makubwa kwani wamezungumza mambo mengi yanayoonesha nia njema katika Nyanja za biashara na uwekezaji baina ya nchi hizo mbili.

“Tunashukuru kwa ujio wa Kaimu Balozi wa Libya nchini kwetu.Kikubwa ambacho Tumezungumza pamoja na mambo mengine kuna moja ya kampuni ya nchi hiyo inataka kuja nchini kuwekeza katika mradi wa umeme wa megawati 400, jambo hili limekuja wakati muafaka ambapo nchi yetu inahitaji sana uwekezaji katika Nishati ya umeme kwa ajili ya matumizi ya viwandani” Alisema Bw.Mshiu.

Aidha Bw.Mshiu ametoa rai kwa wafanyabishara nchini kuitumia TCCIA hasa kwa kuzingatia uwepo wao unalenga kuangalia fursa ambazo wafanyabiashara wanaweza kuzitumia vyema katika kujenga uchumi wa nchi.

“Mwaka huu tunatarajia kusheherekea miaka 30 ya uwepo wa TCCIA. Tumetoa mchango mkubwa katika maendeleo na dhamira yetu ni kuendelea kupanua wigo wa fursa za biashara na uwekezaji nchini, pia tunataka kuthibitisha kuwa tupo kwa ajili ya kuisaidia Serikali katika jitihada za kujenga uchumi,”Alisema.

Kwa upande wake Kaimu Balozi Arze amepongeza jitihada za TCCIA katika kuwaunganisha wafanyabiashara wa Libya na Tanzania, wanatamani kuja kuwekeza hivyo wameona ni vyema kuanza mchakato wa mazungumzo kabla ya kukutana na viongozi wa ngazi mbalimbali Serikalini.

“Kuna maeneo ambayo wafanyabiashara wetu wa Libya wanatamani kuja kuwekeza, hivyo leo nimekuja TCCIA nikiamini kuwa watakuwa sehemu ya kuwaunganisha wafanyabishara wetu. Tunataka pande zote mbili zinufaike na fursa za kibiashara zilizopo,”alisema Kaimu Balozi huyo.

Mkurugenzi wa TCCIA Fatma Hamis amesema nia kubwa la Kaimu Balozi wa Libya ni kuhakikisha sekta ya biashara inapewa kipaumbele kati ya Tanzania na Libya pia kuwaunganisha wafanyabiashara na wawekezaji wa pande zote mbili.

 

Tags: biasharaLibyaTCCIAuchumiumemeviwanda
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Muhogo kupata soko la uhakika China

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In