• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Saturday, June 25, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Usitegemee cha ndugu, utakufa maskini

Patricia Richard by Patricia Richard
May 22, 2018
in FEDHA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Imekuwa desturi katika baadhi ya familia kuwa mmoja wao akifanikiwa kimaisha, basi wote wamefanikiwa. Huyo aliyebahatika ndiye atakayewalisha na kuwavisha huku wao wakiwa hawana tena jitihada za kujikomboa. Ni kweli kuwa katika hali fulani unayejiweza kifedha ndio unalazimika kuwasaidia wengine. Ikitokea kuna watoto, wagonjwa,au wazee wa zaidi ya miaka 65 ni jukumu lako kuwatunza. Lakini hali imekuwa tofauti katika jamii yetu ambapo vijana wamekuwa na jukumu kubwa la kutunza ndugu na familia japokuwa ndio kwanza wanaanza maisha yao.

Kuwabebesha vijana mzigo mkubwa kama huo ni kuwarudisha nyuma kimaendeleo. Jifikirie, kama wazazi wanakutegemea wewe kulipa gharama kama chakula, umeme, maji na wakati mwingine hata ada za shule za ndugu zako unapata wapi nafasi ya kutunza akiba na kuwa na mipango ya baadae? Ni kweli kuwa wazazi wetu wamewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye elimu yetu ili sisi tuje kuwasaidia huko mbeleni lakini hilo linawapa nguvu ya kuziba mipango yako binafsi? Ni sawa kwa vijana kutafuta hela kwa jasho ili tu kulipa gharama za wengine?

ADVERTISEMENT

Wapo wazazi ambao baada ya vijana wao kuajiriwa au kujiajiri, wanakuwepo kwa ajili ya kuwapa ushauri kuhusu namna ya kutumia kile ambacho wanaingiza ile wafaidike. Fikiria fursa ambazo vijana hawa wanazipata. Wanajengewa uhuru wa kufanya maamuzi kuhusu namna wanazoweza kutumia kipato chao kuwekeza katika miradi mingine ya maendeleo ambayo huenda itawaingizia fedha zaidi. Lakini wengine hawana bahati hiyo kwani familia inawategemea wao kwa kila kitu.

Nyakati zinatofautiana na kadri siku zinavyozidi kwenda hali ya maisha nayo inazidi kuwa ngumu. Vijana wakiwa katika mazingira haya wanapata wakati mgumu kujiendeleza na kujitegemea. Kijana ambaye ndo kwanza anapiga hatua hii hapaswi kuona kama ndugu zake wenyewe wanamrudisha nyuma. Hii ni sababu mojawapo ya migogoro ndani ya jamii. Wazazi wasione vijana wao ambao bado ni wachanga katika soko la ajira kama njia rahisi ya kupata fedha. Wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kuwasaidia watoto wao na bila shaka watoto nao watajipanga vizuri na kuwasaidia huku bado wakiwa huru kufanya miradi yao mingine.

Tujenge mazoea ya kusimama wenyewe bila kutegemea wengine katika maisha. Kila mmoja wetu anafanya kazi kwa bidii ili kupambana na ugumu wa maisha hivyo kuwapa vijana majukumu mazito kunawakwamisha kwa kiasi kikubwa kufanya mambo mengine ya msingi na manufaa zaidi. Tufahamu tofauti ya kuomba msaada pale ambapo unakwama na kumtegemea mtu kwa kila kitu. Kama unakwama, omba msaada na kama haujafanikiwa kupata ajira usikae tu kumtegemea ndugu yako, muombe atumie nafasi yake ili kukusaidia wewe kujiendeleza. Jiongeze usikae tu unategemea vitu vya kupewa.

Tags: fedhaSoko la ajira
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Wawekezaji wahakikishiwa ushirikiano

Majaliwa azindua umeme Lindi

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In