• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Tuesday, June 28, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Bila mikopo, wajasiriamali wajiajiri vipi?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 23, 2018
in UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Vijana wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanapiga hatua katika maisha kwa namna moja ama nyingine ili kujikwamua na hali ngumu. Katika miaka ya hivi karibuni, watu wa rika hili wamekuwa wakijiingiza katika shughuli za kilimo, ufugaji pamoja na ujasiriamali. Licha ya jitihada zote za vijana kujikomboa kiuchumi, mikopo kutoka taasisi mbalimbali za kifedha bado inabaki kuwa changamoto kubwa inayowakabili. Wengi wanashindwa kwenda mbali zaidi kimaendeleo kutokana na ukosefu wa mitaji ya kutosha.

Ili wazo la biashara lisibaki kuwa wazo tu, ni lazima mjasiriamali apatiwe mkopo ili afanyie utekelezaji wazo lake na lipate kumlipa na kumuingizia faida. Bila ya kufanya hivyo vijana wengi wataendelea kuwa nyuma kimaendeleo sababu tu wanashindwa kutoka hatua moja kwenda nyingine kwa kukosa mitaji.

Taasisi za kifedha zimekuwa kikwazo kwa vijana wengi kujiendeleza kutokana na masharti magumu wanayoweka hivyo wengi kushindwa kuyatimiza, hali inayopelekea wao kukosa mikopo hiyo kwa ajili ya biashara zao. Kwa vijana wengi wanaojikita na ujasiriamali kumiliki mali isiyohamishika, kuwa na kumbukumbu za taarifa rasmi, wadhamini na hata mali ambazo zinahamishika bado ni vigumu kwa kuwa ndio kwanza wanaanza hivyo wanakosa yote hayo.

ADVERTISEMENT

Inaeleweka kuwa taasisi hizi za kifedha pia zinafanya biashara hivyo ni lazima kuwepo na vigezo na masharti fulani katika utoaji huduma zao. Lakini kwanini kusiwe na mazingira rafiki kidogo kwa ajili ya upatikanaji wa mikopo hii? Hali ilivyo hivi sasa, wengi wanakatishwa tamaa kutokana na ugumu uliopo katika upatikanaji wa mikopo hivyo mawazo yao hubaki kuwa mawazo tu na ndoto zao za kujiajiri huishia hapo.

Ni muhimu kuwa na suluhisho mbadala ambalo litapelekea vijana wengi zaidi kuweza kupatiwa mikopo hii ili kutimiza malengo yao kimaisha. Lengo letu sote ni kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua mbele kimaendeleo hivyo kwanini upatikanaji wa mikopo uturudishe nyuma? Bila ya vijana kupata mikopo hii, hawawezi kuanzisha biashara ambazo zinaweza kuzalisha ajira mbalimbali kwa vijana wengine katika jamii. Na bila ya biashara hizi kusimama serikali nayo inakosa mapato hivyo changamoto hii walionayo wajasiriamali inaathiri jamii nzima kwa kiasi fulani.

Tags: biasharamikopoujasiriamali
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Afya Bora muhimu kwa maendeleo ya nchi

Discussion about this post

Habari Mpya

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 27, 2022

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

by Jensen Kato
June 27, 2022
0

Kilimo biashara kinaendelea kukua barani Afrika na muda umefika kwa watu hususani vijana kuchagamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo. Watu...

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In