• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Friday, September 22, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Afya Bora muhimu kwa maendeleo ya nchi

Patricia Richard by Patricia Richard
May 23, 2018
in HABARI ZA AFRIKA MASHARIKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Afya ni rasilimali muhimu ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa ubora katika shughuli za kila siku kwa mwanadamu yoyote. Bila ya kuwa na afya bora hakuna anayeweza kufanya majukumu yake ya kila siku kwa ustadi na kujiingizia kipato. Watanzania wanatakiwa kuhakikisha kuwa afya zao ni bora ili wawe katika nafasi nzuri zaidi ya kujenga taifa. Lakini haiwezekani kufanya yote hayo bila serikali kuweka msisitizo na kuimarisha huduma za afya.

Ili kuhakikisha kuwa wananchi wake wanakuwa na huduma bora za kiafya, serikali inapaswa kufanya marekebisho makubwa katika sekta hiyo. Takwimu za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka 2016 zinaonyesha kuwa Tanzania ina jumla ya vituo 7,471 vya afya ambapo asilimia 73.7 kati ya hizo zinamilikiwa na serikali huku asilimia 26.3 zikimilikiwa na taasisi au watu binafsi. Lakini je, ubovu wa sekta hii unachangia vipi kudorora kwa uchumi hapa nchini?

Changamoto kubwa inayoikumba sekta ya afya hapa nchini ni msongamano wa watu. Watu hupoteza muda mrefu katika foleni za hospitali, jambo ambalo linapelekea shughuli za kiuchumi kukwama. Ni nini kifanyike ili kupunguza msongamano wa watu hasa katika hospitali za ngazi ya mkoa, rufaa na taifa? Nafikiri serikali ina jukumu la kuhakikisha kuwa zahanati na vituo vya afya hasa vijijini vinatoa huduma inayotakiwa ili kusudi kusiwe na haja ya wagonjwa kwenda kuhudumiwa katika ngazi za juu zaidi.

Pia, ni wajibu wa serikali kuhakikisha kuwa inaongeza idadi ya wanafunzi wanaodailiwa katika masomo ya afya ili kupata wahudumu wengi zaidi katika sekta hii hivyo kuwezesha vituo hivi kutoa huduma kwa urahisi zaidi na kupunguza mzigo kwa madaktari ambao hivi sasa wanahudumia watu wengi zaidi kuliko uwezo walionao. Dawa na vifaa tiba vipatikane kwa urahisi ili kuwezesha wataka huduma kutumia gharama nafuu na muda mfupi kuzipata.

ADVERTISEMENT

Makampuni binafsi na yale ya serikali nayo wanatakiwa kuwajibika ili kujiridhisha kuwa wafanyakazi wake wana afya bora. Moja ya njia ya kufanya hivyo ni kuwakatia wafanyakazi wao bima za afya ili kusudi pindi mtu anapohitaji huduma za kiafya, zinakuwa rahisi kupatikana bila kuingia gharama ya malipo kwa sababu bima waliyokatiwa itagharamia mahitaji hayo yote.

Wafanyakazi pia wanapaswa kufahamu kuwa ni haki yao ya msingi kufanya kazi mahali safi na salama bila ya kuhatarisha afya zao. Mfano mzuri ni makampuni ya ujenzi. Ni wajibu wa waajiri kuhakikisha hawaweki afya za wafanyakazi wao katika hatari yoyote. Usalama katika kazi unapaswa kuwepo wakati wote. Wanaofanya kazi maeneo yenye vumbi nao wasiache kuziba pua na midomo yao kwani kufanya hivyo kunahatarisha afya zao.

Watanzania nao wanapaswa kuzingatia chakula bora. Ni muhimu kula vyakula vinavyojenga na kuupa nguvu mwili pamoja na maji ya kutosha. Jitihada za kujenga taifa haziwezi kuendelea bila kuwa na afya bora. Ni muhimu kutenga muda wa kufanya mazoezi na kupima afya zetu. Kufanya hivyo kutasaidia kugundua tatizo mapema na kupata tiba ili kuendelea na mapambano ya kufanya kazi na kupiga vita umasikini.

 

 

Tags: afyabimaChakula Borahospitaliuchumi
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Watanzania washauriwa kuachana na matumizi ya mkaa

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In