• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, February 5, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Ajali za barabarani zinaturudisha nyuma

Patricia Richard by Patricia Richard
July 6, 2018
in MIUNDOMBINU
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kwa nchi yoyote ile, kupata maendeleo na kujijenga kiuchumi kunatokana kwa kiasi kikubwa na uwepo wa miundombinu bora ambayo inawezesha watu kwenda sehemu mbalimbali pamoja na kusafirisha mizigo yao kwa urahisi hivyo kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya shughuli za kibiashara. Ni vigumu kuwa na maendeleo kama miundombinu hasa barabara hairidhishi. Japo barabara ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa, pia ni chanzo cha vifo vingi hapa nchini pamoja na duniani kote kwa ujumla.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO) inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni moja  hufariki dunia kila mwaka kutokana na ajali za barabarani huku idadi kubwa ya vifo hivi ikitoka bara la Afrika. Ongezeko la vyombo vya moto katika nchi zinazoendelea inatajwa kuwa sababu kubwa ya ajali hizi. Madereva wengi wamekuwa hawazingatii kanuni na sheria za barabarani na matokeo yake taifa inapoteza nguvukazi ya taifa huku ndoto za watu wengi zikizimwa na kupotea pamoja nao.

Je ongezeko la magari hasa katika miji ni ishara ya maendeleo? Madereva wanaosababisha ajali na kuhatarisha maisha ya watu wanachukuliwa hatua za kisheria? Miundombinu yetu nayo inachangia kwa kiasi fulani katika ajali hizi? Maendeleo ya taifa nayo yanaathirika vipi kutokana namatukio ya ajali za barabarani?

Ukweli ni kwamba vijana wengi hupoteza maisha yao kutokana na ajali za barabarani. Vifo hivi mbali na kusababisha upweke na huzuni kwa familia na watu wa karibu pia inarudisha nyuma maendeleo ya wananchi hawa kwa kiasi fulani. Kama aliyepoteza maisha ndio alikuwa tegemezi katika familia je maisha ya familia hiyo yanaendaje baada ya kumpoteza? Ongezeko la ajali nchini Tanzania licha ya kupunguza nguvu kazi ya taifa pia ni kikwazo kikubwa katika maendeleo. Hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa ili kuhakikisha kuwa ajali za barabarani zinapungua na vifo hivi vinaepushwa. Wananchi wanalo jukumu la kufuata sheria za barabarani na kuwa makini pindi wakiwa katika vyombo vya moto.

ADVERTISEMENT

Jamii inapaswa kujenga tabia ya kutii sheria bila shuruti ili kufanikisha lengo hili la kupunguza ajali ya barabarani. Wananchi wanao wajibu wa kutoa taarifa  za madereva wanaokiuka sheria za barabarani kwa  vyombo vya sheria. Serikali inayo inapaswa kuboresha miundombinu hii na kuhakikisha kuwa madereva wanazingatia taratibu zote zilizowekwa. Hatuweki kufikia uchumi wa kati kama nchi itaendelea kupoteza mamia ya wananchi kila mwaka kutokana na ajali za barabarani.

Ili kufikia azma iliyowekwa na serikali inapaswa kuweka mazingira salama yatakayopelekea wananchi kufanya shughuli zao za kimaendeleo bila hofu yoyote. Hivyo basi nguvu zaidi ielekezwe katika kuboresha miundombinu hapa nchini ili kuepukana na matatizo ya ajali na vifo vya barabarani.

 

Tags: AjalimaendeleomiundombinuWHO
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Kuza biashara kupitia mitandao ya kijamii

Discussion about this post

Habari Mpya

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

January 31, 2023
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

January 31, 2023
Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amewataka vijana nchini Tanzania kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo kupitia utekelezaji wa...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amesema kipindi cha mwezi July...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In