• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Kwanini biashara za wanawake haziendelei?

Ukweli ni kwamba, kuanzisha biashara na kuendesha biashara ni vitu viwili tofauti.

Patricia Richard by Patricia Richard
August 26, 2019
in WANAWAKE NA MAENDELEO
0
Tabia hizi zinakurudisha nyuma
Share on FacebookShare on Twitter

Wanawake wamekuwa mstari wa mbele kujiajiri kwa kuanzisha biashara zao na kwa kiasi kikubwa hii imesaidia suala ya kutegemea chanzo kimoja tu cha mapato katika familia. Licha ya hivyo, ukweli ni kwamba, kuanzisha biashara na kuendesha biashara ni vitu viwili tofauti. Wanawake wengi wamefanikiwa kuanzisha miradi yao lakini wachache sana wameweza kuendesha biashara zao kikamilifu hadi kuhakikisha zinafanikiwa.

Hivyo basi, kwanini wanawake wengi wanapata wakati mgumu kuendeleza biashara zao? Tatizo ni nini? Nini kinatakiwa kufanyika ili biashara hizi ziendelee? Ni wapi hasa wanawake wanakwama?

Hizi hapa ni sababu kuu 4 kwanini biashara nyingi za wanawake hufa.

Majukumu ya kifamilia

Wanawake wana majukumu mengi katika familia hivyo inakuwa ngumu kuendesha biashara kikamilifu kwani mara nyingi wanalazimika kushughulikia familia hususani watoto hivyo masuala ya biashara hayapewi kipaumbele ipasavyo. Majukumu mengi ya nyumbani muda mwingine hukwamisha wanawake kutumia muda mwingi zaidi kuhakikisha biashara inakwenda vizuri. Hii ni moja ya sababu kubwa wanawake huamua kuacha kufanya biashara kwani ni ngumu kufanya kila kitu kwa wakati mmoja.

Ili kukabiliana na changamoto hii, unaweza kuomba msaada kwa kushirikisha familia katika kugawa majukumu ili upate muda wa kutosha wa kuendesha biashara na kusimamia majukumu inavyotakiwa.

Elimu ya biashara

Kila biashara inahitaji maarifa na ujuzi. Mara nyingi, wanawake huanza biashara bila kujua wanachohitaji kuendesha biashara hiyo hivyo wanakosa elimu ya mambo muhimu kama vile namna ya kutunza fedha, jinsi ya kushawishi wateja, taarifa za biashara nk.

Mbali na kuwa na elimu ya darasani, elimu ya biashara ni muhimu kwani kuna baadhi ya vitu huwezi kufundishwa shuleni na unapokosa ufanisi na kukabiliana na changamoto nyingi zilizopo katika sekta ya biashara, ni rahisi zaidi kukata tamaa.

ADVERTISEMENT

Ili kuwa katika nafasi nzuri zaidi, hakikisha unafanya utafiti wa kutosha kabla ya kuanzisha biashara yako. Jifunze kupitia semina ambazo huendeshwa bure sehemu mbalimbali, omba ushauri kwa wanawake wengine ambao wamekuwa wakifanya biashara kwa mudamrefu zaidi na pia tumia mtandao kupata maarifa zaidi.

Ubunifu

Asilimia kubwa ya wanawake hawatumii ubunifu wanapoanzisha biashara na badala yake, wanafanya maamuzi kutokana na yale wanayoona katika biashara nyingine. Kama mfanyabiashara ni muhimu kuwa mbunifu kwani utofauti wako ni moja kati ya kivutio kikubwa kwa wateja. Hakikisha unatumia ubunifu wako kujitofautisha sokoni na siku zote epuka kuiga na kufanya maamuzi kutokana na kile unachoona katika biashara nyingine.

Tamaa

Ni rahisi kwa wanawake kuvutiwa na vitu hata kama hawavumudu kifedha. Kutokana na hilo, wengi wao hujikuta wakitumia fedha za biashara kwa ajili ya mahitaji binafsi hivyo kupelekea biashara kuendeshwa kwa hasara na mwisho wake kufungwa kwa sababu faida haionekani. Ni muhimu kuangalia matumizi yako kwa karibu zaidi na kuwa na nidhamu ya fedha ili kufanikiwa katika biashara. Epuka kutumia fedha katika mambo yasiyo na mchango wowote katika kukuza biashara.

Japokuwa kuna vikwazo vingi kwa wanawake wafanyabiashara, inawezekana kabisa kupata mafanikio na kutimiza malengo yako. Endelea kujifunza kila siku na usikate tamaa hata pale mambo yanapokuwa magumu kupita kiasi. Tambua malengo yako na wekeza jitihada kubwa ili kuyatimiza.

Tags: biasharaelimufedhaubunifuwanawake
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Meneja wa Vodacom Tanzania Plc wilaya ya Kinondoni, Suleiman Amri akimsajili Mama Maria Nyerere kwa njia ya alama za vidole nyumbani kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kampuni ya Vodacom Tanzania Plc inaendelea kuunga mkono zoezi hilo lililoainishwa na serikali na kuhamasisha watu wote kujisajili kwa njia ya alama za vidole ambayo ni ya haraka na haina gharama yeyote

Vodacom yaunga mkono serikali usajili wa alama za vidole

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In