• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Kushushwa kwa riba za Benki na mustakabali wa Vicoba

Dennis Msotwa by Dennis Msotwa
June 18, 2018
in BENKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Hivi karibuni Tanzania imepitia mabadiliko makubwa katika sekta ya uchumi na biashara kwa ujumla,mabadiliko haya yamesababishwa na kudorora kwa uchumi na hivyo kusababisha biashara nyingi kufungwa na zingine kusuasua.

 

Moja ya sekta zilizoathirika na hali hiyo ni sekta ya fedha,ikumbukwe hii ni sekta muhimu katika maendeleo ya kiuchumi na ustawi wa nchi kwa ujumla. Fedha ndiyo sekta inayoangaliwa zaidi katika kuchambua vigezo vya ukuaji wa uchumi katika nchi nyingi duniani.Thamani ya fedha ikiwa juu basi na uchumi wa nchi hiyo utakua na kustawi.

 

Mabenki ni moja ya taasisi zilizo katika sekta hii ya fedha na ni waathirika wakubwa wa hali hii ya kiuchumi.Baadhi ya benki zimeanza kuchukua hatua ili kukabiliana na hali hii huku baadhi kama Covenant Bank for Women, Efatha Bank Limited, Njombe Community Bank, Meru Community Bank na Kagera Farmers Cooperative Bank zikifungwa na kuwekwa chini ya uangalizi maalumu wa Benki kuu ya Tanzania(BoT).

 

Katika moja ya hatua zilizochukuliwa na taasisi hizi za fedha ni kushusha riba katika mikopo ili kutoa unafuu kwa wateja wao na pia kuvutia biashara. Hatua hizi zilianzia kwa Benki kuu ya Tanzania ambayo ilishusha riba ya fedha kwa taasisi za mikopo kutoka 16.0% mpaka 9.0% na pia ilipunguza kiwango cha amana zinazotakiwa kuwekwa na taasisi hizo BoT kutoka 10.0% mpaka 8.0%.

 

Hali hiyo ilifuatiwa na benki za CRDB na NMB ambazo nazo zilishusha riba ili kukabiliana na changamoto hiyo. CRDB walishusha riba kwa wafanyakazi kutoka 22% mpaka 16% na kuongeza kiwango cha mkopo kutoka milioni 50 mpaka milioni 100 huku muda wa marejesho ukipaa kutoka miaka 5 mpaka 7. NMB nayo iliamua kushusha riba kwa wafanyakazi kutoka asilimia 21 mpaka 19 na ikishusha riba ya wajasiriamali wadogo kutoka asilimia 23 mpaka 21 na huku ikiongeza muda wa marejesho kwa wajasiriamali wadogo na wakubwa kutoka miezi 60 mpaka miezi 72.

 

Sina shaka ushushaji huu wa riba utakwenda kuvutia wakopaji hasa wajasiriamali wadogo na wafanyakazi ambao wengi wao pia ni wanachama wa vikundi vidogo vya mikopo maarufu kama Vicoba. Wakina mama wengi licha ya kuwa na ajira rasmi baadhi yao ni wanachama wa Vicoba.

 

Waajiriwa hawa wa taasisi za serikali na sekta binafsi zenye mshahara wa kati na mikubwa kulingana na umaarufu na msukumo wa jamii wengi wamejikuta ni wanachama wa Vicoba na ni wakopaji wakuu wakitumia ajira zao kama dhamana ya mikopo hiyo. Wengi hukopa na vikundi huwa na imani ya kuwakopesha kwa maana ya hata biashara zikiyumba basi mshahara utafidia rejesho.

 

ADVERTISEMENT

Kushuka huku kwa riba bila shaka kunaenda kuwavutia wafanyakazi na wajasiriamali hawa ambao wengi ni wadau wa Vicoba na hivyo wataweka msisitizo zaidi katika kurejesha mikopo ya mabenki na Vicoba kudorora. Wadau hawa licha ya kukopa pia ni wawekaji wazuri wa amana(hisa) katika Vicoba vyao kitu ambacho huchagiwa na kipato wanachopata kupitia mishahara yao.hivyo ukopaji katika taasisi zingine za fedha bila shaka kutaathiri ushiriki wao katika vicoba kwa asilimia kubwa.

 

Wajasiriamali na wafanyakazi wawe makini katika kutumia fursa hii ya kushuka kwa riba ili kuepuka mrundikano wa mikopo hivyo kuwawia vigumu kuirejesha na hivyo kuathiri upande mmoja hasa ule ambao njia zake za kukopa zina masharti nafuu.

Tags: ajirabiasharaBoTfedhamikopoRibauchumiVICOBAwajasiriamali
Dennis Msotwa

Dennis Msotwa

Next Post

MV Mwanza kuanza kazi Julai

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In