• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Saturday, June 25, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

NMB Benki kutengeneza ajira 50 kupitia mafunzo kazini

Programu ya mafunzo ya vitendo kazini yazalisha ajira 50

Pesatu Reporter by Pesatu Reporter
December 22, 2020
in BENKI
0
Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Benki ya NMB, Margareth Ikongo akimvalisha kofia mmoja wa wahitimu katika Program ya mafunzo ya uongozi ya Mwaka 2018-20202 ya benki ya NMB

Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Benki ya NMB, Margareth Ikongo akimvalisha kofia mmoja wa wahitimu katika Program ya mafunzo ya uongozi ya Mwaka 2018-20202 ya benki ya NMB

Share on FacebookShare on Twitter

Benki ya NMB kutengeneza fursa za ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu zaidi ya 50 kupitia programu yake maalum ya mafunzo ya vitendo kazini iliyoanzishwa takribani miaka 10 iliyopita.

Mbali na kutoa fursa kwa wahitimu wasio na kazi na sifa zinazohitajika kuajiriwa moja kwa moja, uwekezaji huo umeiwezesha NMB kuzalisha wafanyakazi wenye ujuzi na weledi mkubwa katika maswala ya kifedha na kibenki.

Akizungumza wakati wa mahafali ya wahitimu watano wa mwaka huu wa programu hiyo, Ofisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema mchakato huo si muhimu tu kwa benki hiyo na washiriki wake bali pia kwa tasnia ya fedha na nchi kwa ujumla.

Mahafali hayo yalifanyika makao makuu ya NMB jijini Dar es Salaam na tayari zoezi la kupata wanafunzi wengine 10 watakaoanza mafunzo hayo mapema mwakani yanayochukua miaka miwili limekamilika.

ADVERTISEMENT

“Kama benki inayoongoza kwa faida nchini, tunalo lengo lakutatua changamoto mbalimbali zinazowakumba vijana hususani kwenye masuala ya ajira nchini, hivyo vijana hawa tuliwachukua walivyomaliza kozi mbalimbali vyuoni na kuwapa ujuzi katika maeneo ya kazi ili waweze kuwa na uzoefu wanapoajiriwa,” alifafanua Mponzi.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo Margaret Ikongo ambae ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa NMB, aliyewapongeza wahitimu kwa kuzishinda changamoto walizokumbana nazo baada ya masomo vyuoni.

Alisema hiyo ni mojawapo ya sababu zilizochangia utendaji wao bora na ufanisi kazini mpaka kuajiriwa moja kwa moja na NMB.

“Jinsi mlivyofanya kazi kwa bidii, uvumilivu, juhudi, maarifa, nidhamu na kujituma kipindi cha mafunzo ya  miaka miwili, naomba msiishie hapa tu, bali muende mkalete mapinduzi kwenye kila kazi mnayogusa ili benki yetu iendelee kusonga mbele,” aliwambia wahitimu hao.

Kwa niaba ya wahitimu wenzake, Agnes Nyanzala, alikiri kuyafurahia mafunzo ya vitendo kwa miaka miwili, yaliyojaa uwezeshaji uliowapa urahisi wa kiutendaji, kiasi cha kuivutia NMB na kuwapa ajira.

Nyanzala alisema kuwa kwa sasa wameiva vya kutosha na wana ari kubwa katika kufanya kazi kwa bidii, maarifa na weledi na kwamba wako tayari kwa mamapambano ya kunyanyua ustawi wa NMB kuanzia mwaka ujao wa 2021.

Programu ya mafunzo kazini ya NMB ilianzishwa mwaka 2009 na kila baada ya miaka miwili benki hiyo huwatuma wataalamu wake wa rasilimali watu kwenda vyuoni kutafuta wanafunzi wenye vipaji wapate mafunzo ya vitendo ndani ya benki.

Tags: ajirabenkiBiashara na masokoelimu ya fedhafedhamafunzoNMBwahitimu
Pesatu Reporter

Pesatu Reporter

Next Post
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge akiongea na waandishi wa habari.

Madalali kwenye masoko chanzo wafanyabiashara kupangishiwa vizimba bei juu

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In