• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, February 5, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Mambo matano mjasiriamali anapaswa kujua

Kila mtu ana wazo zuri la biashara lakini wengi wanakwama katika utekelezaji.

Abdul Kassim by Abdul Kassim
December 7, 2022
in BIASHARA NDOGO NDOGO
0
Smiling young African female entrepreneur hard at work on a laptop while sitting at a table in the lobby of a modern office building

Smiling young African female entrepreneur hard at work on a laptop while sitting at a table in the lobby of a modern office building

Share on FacebookShare on Twitter

Ujasiriamali unaendelea kuwa kimbilio la wengi katika harakati za kupambana na ajira. Wananchi wengi wamekuwa wakitambua fursa na kutumia nafasi hiyo kujiajiri ili kumudu maisha.

Japokuwa kundi kubwa la watu wanajikita katika kujiajiri, ni wachache tu ambao wanafikia mafanikio na kutimiza malengo yao. Unaweza kujiuliza, asilimia kubwa wanakosea wapi? Ni vitu gani ambavyo kila mjasiriamali anatakiwa kuzingatia kabla ya kuanzisha mradi wake?

Hapo chini ni mambo matano (5) ambayo kila mjasiriamali anatakiwa kufahamu:

Huwezi kufanya kila kitu mwenyewe

Hakuna mjasiriamali ambaye anapenda kuomba msaada kutoka kwa watu wengine lakini ni muhimu kutambua kuwa huwezi kufanya kila kitu mwenyewe bila msaada wowote. Unaweza kuwa mchapakazi, mbunifu na mwenye malengo makubwa lakini unapofanya kila kitu bila msaada wowote, inaweza kuwa tatizo kwani unakuwa na mzigo mkubwa ambao unaweza kushindwa kubeba siku za mbeleni. Kadri biashara yako inavyokuwa, usisite kuomba msaada na kuajiri watu ambao wana uwezo wa kukusaidia.

Wazo tu halitoshi

Ukweli ni kwamba kila mtu ana wazo zuri la biashara lakini wengi wanakwama katika utekelezaji kutokana na vikwazo mbalimbali. Utekelezaji wa wazo la biashara ndio kitu kinachowatofautisha wajasiriamali duniani kote. Kama unataka kufanikiwa katika sekta ya ujasiriamali, unatakiwa kufanya kazi kwa bidii. Mafanikio hajapatikani kwa sababu ya wazo pekee, unahitaji kufanya mambo mengi ili wazo lako lizae matunda. Wazo lako linatakiwa kuwa mwanzo tu, kama unataka lifanikiwe huna budi kulifanyia kazi usiku na mchana bila kisingizio chochote.

Mapato sio kipimo pekee cha mafanikio

ADVERTISEMENT

Baada ya kuingiza fedha kidogo, ni rahisi kujisahau. Kwa walio wengi, kipimo kikubwa cha mafanikio ni kuingiza kiasi fulani cha fedha/mapato lakini hii haimaanishi kuwa vitu vingine vya msingi havina maana. Jiulize, unabadilisha maisha ya wanaokuzunguka? Unawasaidia wengine kujifunza (wanaweza kuwa wafanyakazi, wateja, wawekezaji) na kuwa bora zaidi? Kuna vipengele vingine muhimu vinavyoashiria mafanikio mbali na utajiri.

Ujasiriamali sio rahisi kama unavyofikiria

Kama unaamini kila kitu unachokiona katika mitandao ya kijamii, basi ni wakati wa kufikiria mbali zaidi. Hatuwezi kukataa kuwa tunaona jinsi wajasiriamali waliofanikiwa wanavyoishi maisha mazuri, wanavyosafiri sehemu mbalimbali duniani na wanavyotumia gharama kubwa kwenye magari, nyumba nk. Lakini tambua kuwa nyuma ya starehe zote hizo kulikuwa na muda mwingi wa kufanya kazi, kushindwa, kufeli na kukata tamaa. Kama sababu pekee ya kutaka kuanzisha biashara ni kuwa tajiri basi upo katika wakati mgumu. Ukweli ni kwamba mafanikio hayapatikani kirahisi kama unavyoona.

Kuwa makini na unaotaka kushirikiana nao

Kufanya biashara na mtu wako wa karibu (familia, rafiki au mume/mke) kunaweza kusababisha athari kubwa. Hii haimaanishi kuwa wote waliofanya hivyo wameshindwa. Kuna ambao wamefanikiwa kufika mbali. Ikifika muda unahitaji mwenzi wa biashara (Business Partner), chukua muda wako na fanya maamuzi sahihi.

Biashara ni kitu kigumu na unaposhirikiana na mtu wa karibu, muda mwingi ni vigumu kufanya maamuzi sahihi bila kuharibu mahusiano hayo. Watu huwa na mawazo tofauti na mara nyingi hii inapelekea kushindwa kuelewana.

Kuanzisha biashara yako mwenyewe ni kitu kizuri sana katika maisha kwani unapata nafasi ya kuleta mabadiliko katika maisha ya watu wengi na jamii kwa ujumla. Kuna faida nyingi za kuwa na biashara lakini pamoja na yote hayo kuna changamoto zake. Mambo yanapokuwa magumu usikate tamaa na badala yake, fanya kazi kwa bidii zaidi, jifunze kutokana na makosa ya nyuma na kikubwa zaidi omba msaada kutoka kwa watu wengine.

Tags: biasharaTanzaniauchumiwajasiriamali
Abdul Kassim

Abdul Kassim

Next Post

Watanzania watakiwa kununua bidhaa za ndani

Discussion about this post

Habari Mpya

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

January 31, 2023
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

January 31, 2023
Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Baadhi ya vijana wakiwa kwenye Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati lijulikanalo kama ‘University Ladies and Gentlemen Conference.

Vijana wahamasishwa kuchangamkia fursa za kilimo

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amewataka vijana nchini Tanzania kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo kupitia utekelezaji wa...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki.

Halmashauri Tanzania zakusanya 485.42 bilioni

by Pesatu Reporter
January 31, 2023
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amesema kipindi cha mwezi July...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In