• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Serikali iimarishe ngazi hizi muhimu za maendeleo

Patricia Richard by Patricia Richard
June 4, 2018
in UWEKEZAJI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Hakuna anayependa kukwama kiuchumi na kubaki katika dimbwi la umaskini. Watanzania wengi ni wachapakazi lakini hawawezi kwenda popote bila uongozi uliopo madarakani kuwapa motisha na kurahisisha njia kwa mtanzania wa kawaida. Wananchi watashindwa kuwa katika nafasi bora zaidi kiuchumi endapo serikali haitachukua hatua katika sekta muhimu ambazo haziepukiki katika shughuli za kiuchumi hasa kwa wananchi wanaoishi vijijini.

Sekta ya kwanza muhimu ni elimu. Hakuna nchi yenye maendeleo bila mfumo bora wa elimu. Shughuli yoyote yenye kuleta maendeleo lazima iende sambamba na elimu bora. Kuna haja ya serikali yetu kuhakikisha vijijini kuna walimu waliofuzu na wanaojitosheleza. Shule zinapaswa kuwa na majengo ya kutosha pamoja na vitabu, maabara na mazingira salama ambayo yatapelekea mwanafunzi kuzingatia elimu tu na siyo vinginevyo.

Katika sekta hii pia, elimu ya ujasiriamali inatakiwa kuanza kutolewa tangu ngazi ya chini. Tatizo la ajira limezidi kukithiri nchini hapa kwa sababu hatujui la kufanya pindi tunapokosa kazi baada ya kumaliza masomo.

Miundombinu pia inapaswa kuboreshwa ili kuwezesha shughuli za kibiashara kufanyika sehemu kutoka sehemu moja au nyingine. Barabara zenye viwango zijengwe kwa wingi vijijini, vivuko navyo vijitosheleze na serikali iangalie uwezekano wa kutoa kodi zisizo na ulazima hapa nchini ili mfanyabiashara apate faida zaidi kutokana na kile anachokifanya. Biashara hutegemea sana miundombinu hivyo bila kuwa na ubora wa hali ya juu katika sekta hii, shughuli mbalimbali za kiuchumi nazo zinakwama.

ADVERTISEMENT

Kama ambavyo ni azma ya serikali kujenga Tanzania ya viwanda, ni muhimu kwa serikali hiyo hiyo kwanza kuinoa sekta ya kilimo. Bila wakulima hapa nchini malighafi zote zinazohitajika ili kujenga Tanzania ya viwanda zitapatikana wapi? Hivyo viongozi wanapaswa kuwa bega kwa bega na kuwaondolea chanagamoto wakulima hapa nchini kusudi malengo yao ya kila msimu yafikiwe.

Hali ya masoko nayo pia iwekewe mkazo. Ili kusaidia wakulima kuuza bidhaa zao na kunufaika na kilimo wanachofanya, ni vizuri kuwepo na soko la uhakika hapa ndani na nje kwa ujumla. Vyama vya ushirika visimamiwe kwa ukaribu zaidi kwani wakulima wengi wanavitegemea. Vitendo vya uongozi mbovu katika taasisi muhimu kama hizi katika maendeleo ya kilimo visiwe vya kufumbia macho.

Serikali ikiboresha sekta hizi, wananchi nao wanafarajika na kupata nguvu zaidi wakiwa wanatekeleza wajibu wao wa kujenga taifa. Serikali kupitia wizara zake mbalimbali inapaswa kuwa sikivu na kuelewa wananchi wake hivyo kujua jinsi gani ya kuwawekea mazingira bora kiuchumi.

Tags: biasharaelimumaendeleoujasiriamaliviwanda
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Businessman checking stock market on tablet

TEHAMA: Fursa mpya ya kukuza uchumi

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In