Home Elimu Unesco kuendesha mafunzo kwa radio 25

Unesco kuendesha mafunzo kwa radio 25

0 comment 25 views

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) litaendesha mafunzo kwa vituo vya radio 25 nchini Zanzibar kuanzia leo hadi Julai 18 mwaka huu.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha waandishi wa habari wa radio na watangazaji kutengeneza vipindi vya maendeleo huku vikizingatia jinsi.

UNESCO itawajengea uwezo waandishi wa habari kuwa na uwezo wa kutengeneza taarifa za habari zenye uhusiano na maendeleo na jinsi.

Aidha radio zote zinazoshiriki zitapatiwa kiasi cha fedha kutumika katika kuboresha uzalishaji wa vipindi na taarifa za habari kwa kuzingatia jinsi na maendeleo kwa muda wa miezi sita.

Lengo kuu la kuboresha vipindi hivyo ni kuwezesha zaidi sauti za wanawake kusikika kupitia vipindi mbalimbali vya mahojiano.

UNESCO kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uswisi linaendesha mradi wa kuwezesha radio za wananchi kuwa na  mifumo ya tehama inayosaidia kutengeneza vipindi vizuri na vyenye kuwezesha maendeleo endelevu nchini.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter