Kampuni ya Vodacom imefanikiwa kutoa gawio la Sh.83.81 kwa kila mwanahisa wake baada ya kupata faida ya takribani Sh.170.24 bilioni kwa mwaka ulioishia Machi 31. Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Ian Ferrao amesema kampuni hiyo imefanikiwa kutengeneza faida kubwa katika maeneo matatu ambayo ni huduma, mauzo ya data pamoja na M-Pesa. Ferrao ameeleza kuwa wamepata mafanikio hayo kutokana na kuboresha huduma wanazotoa kwa wateja na kuimarika kwa matumizi ya data na mfumo wa fedha ambao unaboreshwa mara kwa mara.
Tanzania yaikaribisha kampuni za China kuwekeza Sekta ya Nishati
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Tanzania,...
Discussion about this post