• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Mkurugenzi Mpwapwa abanwa kutoa fedha za mikopo ndani ya siku 10

Patricia Richard by Patricia Richard
October 11, 2018
in MIKOPO
0
Majaliwa ataka benki kushusha riba

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Share on FacebookShare on Twitter

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku 10 kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa, Bw. Peter Swea awe ametoa fedha za mikopo kwa ajili ya vijana, wanawake na walemavu.

“Leo (jana) ni tarehe 10 nataka hadi ikifika tarehe 20 ya mwezi huu uwe umeshatoa fedha za mikopo kwa wanawake, vijana na walemavu. Habari za mpaka kikao kiridhie hayo ni mambo ya zamani na ndio maana ikatungwa sheria kwa ajili ya jambo hilo. ”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Jumatano, Oktoba 10, 2018) wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Kibakwe wilayani Mpwapwa mara baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kibakwe, akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Dodoma. Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya Mkurugenzi huyo kumueleza kuwa bado hajatoa fedha kwa ajili ya mikopo hiyo ambazo alipaswa kuzitoa kila robo mwaka, akidai bado kikao cha kuidhinisha hakijakaa.

Amesema fedha hizo ambazo ni asilimia 10 ya mapato ya ndani yanayokusanywa kwenye halmashauri, ambapo anatakiwa kutumia asilimia nne kwa ajili ya mikopo ya wanawake, asilimia mikopo kwa ajili ya vijana na asilimia mbili zitolewe kwa walemavu.

Kadhalika,Waziri Mkuu amewaagiza watendaji wote wa vijiji kuainisha maeneo yote yenye misitu na vyanzo vya maji pamoja na kuwachukulia hatua kali watu wote watakaobainika kukata miti bila kibali.

ADVERTISEMENT

Amesema mtu yeyote atakayebainika kukata miti bila kibali achukuliwe hatua kali kwa sababu wamekuwa wakisababisha ukosefu wa maji, ambapo wakandarasi wa maji kwenye wilaya hiyo wanapata changamoto ya kukosa maji kwenye maeneo mengi wakati awali, Mpwapwa ilikuwa na ardhi ya chepechepe.

“Nimepata habari, hapa Kibakwe watu wanakata miti ili kushindana ubavu wao wa kuishi. Nawaagiza watendaji wote wa vijiji kuainisha maeneo yenye vyanzo vya maji na misitu na muyalinde. Madiwani pia mnatakiwa kushiriki kukemea ukataji miti.”

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Bw. Jabir Shekimweli ameishukuru Serikali kwa kutenga Sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vitatu vya afya ambavyo ni Kibakwe, Mima na Pwaga. Amesema miradi hiyo imesimamiwa vizuri na kamati za ujenzi kwenye kata na vijiji husika kama ambavyo muongozo ulivyoelekeza.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Bw. George Simbachawene amesema utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) umefanyika kwa mafanikio makubwa kwenye sekta ya afya, umeme na elimu. Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, ameomba ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Kongwa, Mpwapwa hadi Kibakwe, uharakishwe ili kuondoa adha ya miundombinu inayowakabili wananchi.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU

Tags: DodomafedhaKassim Majaliwamikopovijanawanawake
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Selemani Jafo.

Mtendaji Mkuu mabasi mwendokasi aonywa

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In