• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Vidokezo muhimu vya fedha kwa vijana

Ni muhimu kuwa na bima ili kujilinda na kulinda mali zako.

Leah Nyudike by Leah Nyudike
July 25, 2019
in FEDHA
0
Punguza gharama kwa kufanya haya
Share on FacebookShare on Twitter

Kwa bahati mbaya elimu kuhusu fedha binafsi huwa haitolewi katika shule na vyuo vingi. Kutokana na hilo vijana wengi hukosa elimu ya msingi  kuhusu fedha hivyo kuwafanya wakose matumaini kuhusu jinsi ya kudhibiti fedha zao, kuomba mikopo, na vilevile kujiepusha na madeni.

Kama kijana, ili kuelewa zaidi masuala ya fedha na kuishi maisha mazuri yenye mafanikio ni muhimu kujua vidokezo vifuatavyo;

Jifunze kujizuia

Kuna baadhi ya vijana ambao wamebahatika kufundishwa na wazazi wao kuhusu kujizuia walipokuwa watoto. Hivyo kama hukufundishwa ni muhimu kujua kadri utakavyowahi kujifunza kujizuia ndivyo mabadiliko yatakavyotokea katika masuala yako ya kifedha. Hivyo jenga tabia ya kulipa fedha taslimu kwa vitu unavyohitaji/vya muhimu. Pia epuka kukopa ikiwa huna sababu maalum.

Dhibiti mustakabali wako wa kifedha

Ikiwa hutajifunza kusimamia fedha zako mwenyewe, watu wengine watatafuta njia ya kusimamia fedha zako. Baadhi ya watu hao wanaweza kuwa na nia mbaya, na wengine wanaweza kuwa na nia nzuri lakini watakuwa wanajua mapungufu yako. Badala ya kutegemea ushauri kutoka kwa watu wengine, chukua hatua na anza kwa kujisomea vitabu kuhusu masuala ya fedha binafsi. Siku zote kuelewa fedha zinavyofanya kazi huwa ni hatua ya kwanza ya kuzifanya fedha hizo zikufanyie kazi. Ikiwa unataka maisha yako ya baadae yawe mazuri basi ni muhimu kujua fedha zinavyofanya kazi na sehemu ya kuziweka ili ziweze kuzalisha faida.

Jua fedha zako zinakwenda wapi

Baada ya kupata elimu ya msingi kuhusu masuala ya fedha binafsi, ni dhahili kuwa utaona kuwa kuna umuhimu wa gharama za matumizi yako kutokuzidi mapato yako. Na njia bora ya kuwezesha hilo kufanyika ni kuweka au kutengeneza bajeti. Pia hakikisha gharama zako za mwezi zipo chini. Ikiwa hutopoteza fedha zako kukaa katika ghorofa la kifahari sasa unaweza kumiliki nyumba nzuri zaidi muda si mrefu kwa sababu ya bajeti.

Anzisha mfuko wa dharura

Moja ya mambo ambayo hurudiwa kila siku ni pamoja na “kujilipa kwanza” bila kujali una madeni kiasi gani, au una mshahara mdogo kiasi gani. Ni muhimu kutafuta kiasi chochote katika bajeti yako na kukiweka katika mfuko wa dharula kila mwezi.

Anza kuweka akiba

Ni muhimu kwa kila kijana kufikiria maisha baada ya kustaafu. Hivyo kwa kuanza mapema kuweka akiba, kutakusaidia kuwekeza na kuweza kupata fedha kwa ajili ya maisha baada ya kustaafu. Kuna baadhi ya kampuni hufadhili mipango ya kustaafu mara nyingi mipango hiyo huwa na mikakati rafiki kwa wafanyakazi hivyo sio vibaya kujiunga nayo.

ADVERTISEMENT

Kuwa na uelewa wa masuala ya kodi

Hata kabla hujapata mshahara wako wa kwanza ni muhimu kujua mambo kadhaa kuhusu kodi. Wakati kampuni inakupa mshahara, unahitaji kujua jinsi ya kuhesabu ikiwa mshahara huo utakupa fedha za kutosha baada ya kodi kufikia malengo. Bahati nzuri siku hizi unaweza kufanya mahesabu hayo kupitia mtandao na kujua kiasi gani kinakwenda katika kodi.

Linda afya yako

Ikiwa kufikia malipo ya bima kwa mwezi ni jambo lisilowezekana, Je utafanyaje ikiwa unatakiwa kwenda katika chumba cha dharura kwa sababu ya magonjwa ambayo hukupanga kupata? Kama huna bima ya afya ni muhimu kuipata ili kuweza kurahisisha gharama ikiwa ajali au magonjwa yatakupata. Unaweza kujipatia bima ya afya kwa bei nafuu kutoka NHIF.

 

Tags: bajetibimaelimufedhakodimikopouchumi
Leah Nyudike

Leah Nyudike

Mwandishi

Next Post
Je, wajua haya kuhusu kahawa?

Je, wajua haya kuhusu kahawa?

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In