• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Kazi ya ndoto yako au Kazi ya kuingiza kipato tu?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 30, 2018
in HABARI ZA AFRIKA MASHARIKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Ajira imeendelea kuwa changamoto kubwa wa watu wengi. Kuna ambao wamebahatika na kupata kazi ambazo huenda zinawalipa vizuri tu lakini bado hawazifurahii. Hali hii ipo kote duniani sio hapa kwetu pekee. Kundi kubwa la waajiriwa wanafanya kazi ambazo hawazifurahishi sababu tu zinawawezesha kumudu familia na maisha kwa ujumla. Wachache sana hutafuta na kupata kazi ambazo wanazipenda na kuzifurahia. Soko la ajira limechangia kwa kiasi kikubwa katika tatizo hili kutokana na ugumu wake. Wengi huishia katika kazi ambazo wanazifanya tu ili walipwe na waweze kukabiliana na ugumu wa maisha.

Kama kundi kubwa la waajiriwa wapo katika nafasi zao ili tu kujikumu huduma wanazotoa zinaathirika kwa namna yoyote ile? Wanakuwa na moyo wa kutoa huduma kwa haki na usawa? Wanajali kuhusu wale wanaowahudumia? Wanazingatia haki za msingi za wataka huduma wao? Au yote haya sio muhimu kwa sababu tu mwisho wa siku wanapata kipato chao?

Lakini ni muhimu kujiuliza mzizi haswa wa tatizo hili ni nini? Ugumu wa maisha umepelekea watu kukubali kufanya kazi yoyote? Kwanini ni asilimia ndogo tu ya watanzania wanafurahia ajira zao na kutekeleza majukumu yao kwa moyo mmoja?

ADVERTISEMENT

Suala hili linapaswa kuangaliwa na kupewa uzito kwani kuna baadhi ya sekta kama vile elimu, afya na fedha zinawagusa wananchi moja kwa moja hivyo huduma isiyoridhisha inaweza kumuathiri mtu kwa kiasi kikubwa. Ni kweli kwamba ili kutimiza wajibu wako sehemu ya kazi ni lazima uwe na ujuzi, elimu na uzoefu unaotakiwa lakini kuna sababu ya kutoa elimu kwa umma hasa kwa jamii kama vile wanafunzi ili kuwafundisha umuhimu wa kupenda kile unachofanya. Kufanya hivi kutawatayarisha mapema kabla hawajaingia rasmi katika soko la ajira.

Ni kweli kwamba tunahitaji kipato kizuri ili kuweza kuendesha maisha yetu na kumudu mahitaji mbalimbali ya familia. Hakuna anaeweza kubishana na hilo. Lakini ongezeko kubwa la watu kufanya shughuli yoyote tu ambayo itawasaidia kujikimu halipaswi kufumbiwa macho. Kuna ugumu katika kupata kazi unayopendelea au kiwango cha mshahara ni kidogo? Fikiria, kama wahitimu mia moja (100) wa tasnia fulani wakiachana na kazi ambayo wameisomea na kutafuta kazi nyingine ambayo inalipa vizuri taifa inapoteza wataalamu wangapi kila mwaka?

Mwisho wa yote kipato unachopata ndicho kinaendesha maisha na sio vinginevyo. Lakini ni vizuri kuwepo na uwiano baina ya mambo haya mawili ili kuhakikisha kuwa japokuwa unaingiza kipato kizuri kinachofanikisha malengo yako mengine ya maisha, bado una heshima na nidhamu na kazi unayofanya na unatoa huduma stahiki kwa walengwa au jamii kwa ujumla.

Tags: ajiraFamiliaHuduma'Kipato
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Benki zilizoshusha riba zapongezwa

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In