• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Thamani ya ufundi stadi isionekane baada ya kufeli

Patricia Richard by Patricia Richard
June 4, 2018
in UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Katika jitihada za kufanikisha azma ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ni vizuri kama elimu ya ufundi stadi ikapewa thamani na umuhimu kubwa. Mara nyingi hapa nchini, ufundi stadi umeonekana kama suluhisho la mwisho kwa vijana ambao wamekata tamaa na maisha. Vyuo vinavyotoa elimu hii vimekuwa havipewi kipaumbele katika jamii. Lakini ukweli ni kwamba, taasisi kama hizi zinatoa mchango mkubwa sana katika maendeleo ya taifa.

Unaweza kujiuliza kwanini wananchi wengi huona aina hii ya elimu kama kimbilio lao baada ya jitihada nyingine zote kufeli. Kwanini watanzania hawavipi heshima vyuo au taasisi kama hizi? Na je, ni nini taasisi kama hizi zinafanya ili kubadilisha mitazamo hii jamii iliyonayo? Serikali nayo inatoa msaada gani kwa sekta hii ili kuiboresha kama ilivyo kwa hizo nyingine?

ADVERTISEMENT

Ukweli ni kwamba taasisi za ufundi stadi zimekuwa na mchango mkubwa sana katika kubadilisha maisha ya watu na kuleta maendeleo hapa nchini. Mfano hai wa hili ni Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi Tanzania (VETA). Mamlaka hii imebadilisha maisha ya mamia ya watanzania hasa vijana kutokana na mafunzo yake.

VETA imesaidia vijana wengi katika jamii kuweza kujiajiri na kujiingizia kipato. Wengi hasa wale ambao hawakupata nafasi ya kuendelea na masomo yao wamekuwa wakijiunga na mamlaka hii iliyo na matawi mengi kote nchini ili kujiendeleza kielimu pamoja na kiuchumi badala ya kukaa tu mitaani bila shughuli yoyote.

Kupitia ufundi stadi pia, vijana wengi wamefanikiwa kujifunza na kujikita katika ujasiriamali ili kujikwamua na umaskini. Mfumo huu wa elimu umekuwa kama tumaini jipya kwa wengi ambao ndoto zao za kujiunga na elimu ya juu hazikutimia. Vijana hawa wamepata fursa nyingine ya kutimiza ndoto zao na kubadili maisha yao kiuchumi. Vijana hawa pia kwa kujiajiri, nao wamefungua milango ya ajira kwa watanzania wengine na hivyo wamesaidia kupunguza tatizo la ajira hapa nchini.

VETA imekuwa na lengo la kuwawezesha watanzania kushiriki kiutendaji katika sera ya uchumi wa viwanda kupitia mafunzo mbalimbali wanayotoa. Mamlaka hii imewapa fursa vijana wengi hapa nchini na imekuwa ikiendelea kufanya hivyo. Mwaka uliopita, mamlaka hii ilishirikiana na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel na kuzindua VSOMO, mfumo wa utoaji elimu ambao utawezesha wananchi kujifunza kupitia simu ya mkononi.

Serikali pamoja na wadau wengine wa maendeleo kutoka sekta binafsi wanatakiwa kupaza sauti zao na kusaidia mamlaka kama hizi katika shughuli zao za kuwafikia watanzania wengi zaidi. Jamii ikipata mtazamo mzuri wa mamlaka hizi bila shaka vijana wengi zaidi watajiunga nazo na hivyo kuchangia moja kwa moja katika maendeleo ya taifa letu.

Tags: ajiraelimumaendeleouchumiUfundi StadiVETA
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Magufuli awasha moto TADB

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In