• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Wazo lako ajira yako

Patricia Richard by Patricia Richard
May 26, 2018
in UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Idadi kubwa ya watanzania wamejiajiri. Ujasiriamali umezidi kuwavutia watu wengi hasa vijana ambao baada ya masomo wamekuwa wakifikiria kujiajiri badala ya kutafuta ajira. Ili kufanikiwa katika shughuli yoyote ambao unatarajia kufanya jambo la muhimu kuliko yote ni kuwa na wazo zuri la biashara. Hata kama una mtaji wa kutosha huwezi kufika mbali kibiashara kama wazo lako halijitoshelezi. Wengi hushindwa katika hatua hii muhimu kuliko zote na kupelekea biashara zao kushindwa kusimama kwa muda mrefu. Hapo chini ni baadhi ya mbinu ambazo unaweza kutumia ili kupata wazo bora la biashara.

Kwanza kabisa inatakiwa kujenga biashara yako kutokana na ujuzi ulionao. Biashara kamwe haitofika juu kama unafanya kitu ambacho hauna uelewa nacho. Ni vizuri kujenga biashara yako kutokana na ujuzi na uzoefu ulionao. Kama unafahamu vizuri kuuza duka basi anzisha duka lako mwenyewe, kama ulishawahi kufanya kazi katika mgahawa basi anzisha wa kwako mwenyewe. Ni muhimu kuwa na uelewa wa kutosha wa kile unachotarajia kufanya kabla ya kusimamisha biashara yako.

ADVERTISEMENT

Inapaswa kuangalia nini jamii inayokuzunguka inahitaji kabla ya kuanzisha biashara yoyote ile. Kufanya hivyo kutasaidia kufahamu ushindani uliopo, kujua jinsi ya kuvutia soko na pia kuangalia kama wazo lako linalipa mahali ulipo. Kama umezungukwa na biashara za mbogamboga na wewe ukafungua kitu hicho hicho hutakuwa na uhakika na biashara hiyo kwa sababu watu kumi tayari wanaifanya. Hivyo ni muhimu kuangalia ni nini jamii yako inakosa na kutengeneza wazo lako la biashara kutokana na mapungufu hayo.

Angalia mfumo wa maisha ulivyo. Kama mjasiriamali unapaswa kufikiria kuwa watu wanaokuzunguka ndiyo wateja wako watarajiwa. Hivyo ni muhimu kuangalia maisha yao ya kila siku na kupata wazo lako kutokana na jinsi maisha yao yanavyoenda. Huwezi kuanzisha kibanda cha simu mahali ambapo unaona kila mtu anamiliki simu tayari sababu hakuna atakayehitaji huduma hiyo. Kama jamii yako ni ya maisha ya chini anzisha biashara ambayo wanaweza wakaimudu na siyo ambayo itakuwa juu ya uwezo wao wa kiuchumi. Kama umezungukwa na hospitali kwa mfano una nafasi nzuri ya kuanzisha duka ka madawa na kufaidika kutokana na mazingira kuwa rafiki kwa aina hiyo ya biashara.

Pia unaweza kuchukua wazo la biashara ambalo tayari lipo na kuliboresha kulingana na mahitaji ya eneo unalotarajia kufanya biashara yako. Watu wengi hutumia mbinu hii kwani ni rahisi kutambua nini hasa wanaweza kufanya kwa kuangalia nini wajasiriamali wengine wamefanya na kufanikiwa. Unaweza kuangalia mitandao ya kijamii au hata kupitia tovuti mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi na kuona biashara gani zimefanikiwa zaidi. Baadaye unaweza kuziboresha ili kukudhi mahitaji ya mazingira yanayokuzunguka.

Wazo la biashara ndiyo hatua ya awali kabisa na inahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kufahamu ni nini hasa kinahitajika. Wazo lako ndiyo mtaji wako wa kwanza. Wekeza muda wa kutosha katika hatua hii na utaona matunda yake baadaye. Baada ya kupata wazo lenye tija kwako pamoja na jamii kwa ujumla ndipo unaweza kuanza kutafuta mtaji na kubadili wazo lako kuwa ajira yako.

Tags: ajirabiasharaMitandao ya kijamiimtajiujasiriamali
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Panya wavamia mashamba Pwani

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In