• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Viwanda vidogo vinajiandaa vipi kuelekea Tanzania mpya ya viwanda?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 26, 2018
in VIWANDA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Tangu serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani sekta ya viwanda imeboreshwa na kufanyiwa mabadiliko kwa kiasi kikubwa. Serikali imeweka azma ya kufanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ili kuimarisha uchumi wake na kuzalisha ajira zaidi kwa vijana. Dhamira hii imeonekana kukubaliwa na kuungwa mkono na sekta mbalimbali hapa nchini. Lakini kabla ya kufikiria matunda yote yatakayotokana na uchumi wa viwanda inapaswa kujiuliza, viwanda vidogo pamoja na vile vya kati vimejipangaje kuelekea Tanzania hii mpya?

Ni dhahiri kuwa ili kukuza uchumi wa nchi kwa kupitia sekta ya viwanda ni lazima kutambua changamoto zilizopo katika sekta hii na kutafuta suluhisho la kudumu. Pia inatakiwa kufahamu kuwa asilimia kubwa ya viwanda hapa nchini ni vidogo na vya kati hivyo lazima kuwepo na mazingira mazuri yatakayopelekea viwanda hivi kuweza kuendelea na kuongez kasi ya uchumi wa viwanda.

Inatakiwa kujiuliza, viwanda vidogo na vile vya kati vimejipanga vipi kukabiliana na kasi ya serikali ya awamu ya tano katika kuinua uchumi nchini? Viwanda hivi vidogo vinapata misaada yoyote kutoka kwa serikali au wadau mbalimbali ili kuongeza mitaji yao, kuongeza maarifa yao pamoja na kuongeza uzalishaji wao? Serikali imefanya jitihada zozote ili kutatua changamoto zinavyopelekea viwanda hivi kuendelea kuwa katika hali ya chini?

Pia kuwe na mazingira mazuri ili kuvutia wawekezaji wa nje na hata hapa ndani. Kuweka mazingira mazuri ya kuwekeza katika viwanda vidogo ni njia moja wapo ya kuinua viwanda hivi na kuvisaidia kuendelea na kupiga hatua kimaendeleo. Wawekezaji wengi wamekuwa wakikimbilia kuweka fedha zao kwenye miradi mikubwa huku wakiviacha nyuma viwanda vidogo kutokana na kuwa katika mazingira ambayo sio mazuri kama ilivyo kwa viwanda vikubwa.

ADVERTISEMENT

Ili kwenda sambamba na kasi ya maendeleo kupitia sera ya viwanda kama ambavyo serikali imedhamiria, ni vizuri kama viwanda vidogo vikitumia rasilimali walizonazo kuhakikisha kuwa bidhaa wanazozalisha zinazingatia viwango na ubora ili vipate fursa ya kustahimili ushindani katika soko la kitaifa. Bila ya kuwa katika ubora wa hali ya juu bidhaa hizo hazitofanya vizuri sokoni na hali hiyo inaweza kupelekea baadhi ya viwanda vidogo kushindwa kujiendeleza.

Sera hii ya kubadilisha Tanzania kuwa nchi ya viwanda imepokelewa kwa mikono miwili katika jamii zetu. Lakini ni vizuri kama serikali kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali pamoja na wadau wa masuala ya maendeleo ikiendelea kuelekeza nguvu nyingi zaidi kuinua viwanda vidogo ili vipate kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujiendesha na kukabiliana na Tanzania hiyo mpya. Kuviacha nyuma viwanda vidogo haitasaidia kasi ya uchumi ya viwanda hapa nchini kwani watanzania wengi nao watakuwa wameachwa nyuma.

Tags: fedhaRasilimaliuchumiviwandawawekezaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Wazo lako ajira yako

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In