• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Umemfungulia mwanao akaunti ya benki?

Patricia Richard by Patricia Richard
August 20, 2018
in BENKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia watanzania wengi zaidi wakijiunga na huduma za kibenki kutokana na jitihada mbalimbali ambazo taasisi za fedha zimekuwa zikifanya katika kuhakikisha wananchi wanaelimika na kuhamasika kuanza kutumia mifumo rasmi ya utunzanji wa fedha huku wakiachana na ile waliyoizoea.

Japokuwa suala hili limeonyesha mafanikio kwa kiasi kikubwa, bado kuna changamoto ambazo sio rahisi kuzifumbia macho. Japokuwa idadi kubwa ya wananchi wamebadili mtazamo na kuanza kutumia mifumo rasmi kutunza fedha zao, watoto wameonekana kusahaulika katika mabadiliko haya.

Asilimia kubwa ya wazazi, walezi au hata wananchi wa kawaida wanadhani kuwa labda huduma za kibenki zipo kwa ajili ya watu wazima tu, yaani wale wote waliotimiza miaka 18 na kuendelea ambao kisheria wanatambulika kama watu wazima. Ingawa taasisi mbalimbali za fedha zimekuwa na programu maalum kwa ajili ya watoto chini ya umri wao, wengi wanaonekana kutokuwa na taarifa au maarifa kuhusu huduma hii muhimu ambayo imeanzishwa hususani kwa ajili ya watoto.

Kwa upande wao, Benki ya NMB inayo akaunti maalum inayofahamika kama NMB Mtoto Akaunti ambapo walengwa wakuu ni watoto japokuwa kisheria inaendeshwa na ipo chini ya wazazi au walezi. Akaunti hii inalenga kutunza akiba ya mtoto na kiwango chake rafiki cha riba kinawezesha akiba kuendelea kukua. Mbali na masuala ya riba, NMB Mtoto Akaunti inafunguliwa kwa kiasi kidogo cha Sh. 10,000 tu za kitanzania hivyo gharama hii ndogo inaruhusu wazazi/walezi kutoka hata familia zile za chini kumudu gharama na kuwekeza kile kidogo walichonacho kwa ajili ya watoto wao.

ADVERTISEMENT

Kama mzazi/mlezi unaweza ukawa unajiuliza ni kwanini hasa ufungue akaunti kwa ajili ya mtoto/watoto wako? Kwanini usiwatunzie akiba katika akaunti yako binafsi? Ni kwa sababu gani ufanye hivyo japokuwa hawatoweza kutumia fedha hizo kwa wakati huo? Maswali haya ni baadhi tu katika yale mengi ambayo labda wazazi hujiuliza wanapoambiwa kuwa hata watoto nao wanaweza kufunguliwa akaunti za benki.

Ukweli ni kwamba kuna faida nyingi tu za kufanya hivyo. Kwa taasisi ya NMB, programu yao ya watoto akaunti mbali na kutoa riba ambayo humpa mteja zaidi, pia inasaidia kumjengea mtoto nidhamu ya kutunza fedha na kuwa na akiba ambayo itamsaidia katika maisha ya baadae. Akiba ya mtoto pia inampatia uhakika wa masuala muhimu kama elimu, afya na ustahimilivu wa maisha. Kuweka akiba pia kunamsaidia mtoto kupanga matumizi yake mwenyewe pindi anapofikia umri wa kumiliki fedha zake kihalali.

Kama wanavyofanya NMB, benki nyingine zinapaswa kuwa na akaunti maalum kwa ajili ya wazazi kuweka akiba ya watoto wao na isiishie hapo tu, wanapaswa kuingia mitaani na kuwaelimisha wananchi hususani wale wenye maisha ya kati na ya chini kuhusu umuhimu wa kuwa na akiba ya watoto kwani kufanya hivyo ni mojawapo ya kuwahakikishia kuwa watapata mahitaji yao ya msingi huko baadae.

Vilevile, jukumu hili lisibaki kwa taasisi za fedha pekee. Wazazi na walezi wanapaswa kujenga mazoea ya kuzungumza na watoto wao kuhusu hali yao ya kifedha. Katika ulimwengu huu wa utandawazi ni muhimu sana kwa wazazi kuwa huru kuzungumza masuala ya kifedha na watoto wao. Kwa kufanya hivyo, watoto nao wanapata ufahamu kuhusu namna ambazo wanaweza kusaidia kutunza fedha, kujiwekea akiba na hata kuwasaidia wazazi wao pale wanapoweza. Jamii kwa ujumla inapaswa kubadilika hasa katika mambo yanayohusu fedha na wazazi kujitokeza kwa wingi kufungua akaunti kwa ajili ya watoto wao ni hatua kubwa kuelekea ulimwengu mpya kabisa wa huduma za kibenki na faida zake lukuki.

Tags: akibabenkifedhaNMBNMB Mtoto AkauntiRiba
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Fursa 5 za kiuchumi Dodoma

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In