• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Tuesday, June 28, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Umri usiwe kikwazo cha maendeleo

Patricia Richard by Patricia Richard
June 22, 2018
in HABARI ZA AFRIKA MASHARIKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Katika maisha kuna ambao wanabahatika kuwepo katika mazingira mazuri ambayo yanapelekea njia yao ya maendeleo kuwa rahisi na bila vikwazo vyovyote hivyo wanakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujiendeleza kimasiha hasa katika masuala ya uchumi. Lakini vile vile kuwa wale ambao hawakupata bahati hiyo. Mazingira waliyoyakuta yaliwalazimu kupambana ili kutoka kimaisha. Hawa ni wale ambao hawali kama hawajahangaikia chakula chao. Kundi kubwa la watanzania wanaangukia hapa. Wengi wamelazimika kufanya kila kitu kwa bidii kubwa ili kuona matunda ya jasho lao. Lakini hadi kufikia hatua hiyo umri wa watu hawa unakuwa umeenda kwa kiasi kikubwa na wengine huona kama ni wakati wa kupumzika hivyo wanafunga milango yote ya kuwaingizia riziki.

Umri haupaswi kuwa kikwazo katika maendeleo ya mtu. Ukweli ni kwamba kuna watu wazima walio na umri wa miaka hadi thelathini wanasoma vyuoni. Hawa ni wachache walio na ujasiri wa kukubali kwamba, kutokana na sababu mbalimbali hawakupata fursa ya kujiendeleza kielimu hivyo walichukua muda zaidi kufika hapo kuliko wengine. Hili sio jambo la aibu japokuwa wengi katika jamii zetu wamekuwa na mazoea ya kutumia umri kama kikwazo katika kujiendeleza kimaisha.

ADVERTISEMENT

Wengi wamejenga taswira ya kwamba unapaswa kuwa katika nafasi fulani kimaisha kabla hujafikia umri fulani. Taswira hii imekuwa ikiwapotosha wengi na kuwafanya waone kama hawana tena nafasi ya kujiendeleza kielimu au hata kiuchumi ili wapate kuwa katika nafasi nzuri zaidi. Jamii zetu zimekuwa hazitoi ushirikiano wa kutosha kwa makundi haya ya watu. Ni nani alisema kuwa huwezi kuendelea na elimu ukifika umri fulani? Ni kwa sababu gani watu hawa hawapewi nafasi wanayostahili katika kujenge taifa letu? Tangu lini umri umekuwa kikwazo katika masuala ya maendeleo?

Soko la ajira nalo linapaswa kutoa fursa sawa ili watu hawa wasiachwe nyuma. Kwasababu tu umri umeenda haimaanishi kuwa mtu hapaswi kunyimwa ajira. Kama vigezo vyote vinavyohitajika vipo haina maana kuweka ugumu kwa watu hawa kwani wanayo haki ya kuajiriwa kama walivyo wengine mradi tu wanakidhi matakwa yanayotakiwa. Watu hawa wanapaswa kupewa heshima wanayostahili kwa maarifa walionao na mchango wanaouleta katika jamii sio tu kwa umri walionao.

Sio jambo la aibu kujiendeleza hata kama umri wako umeenda. Kama unao uwezo wa kufanya hivyo ni vizuri kuweka bidii katika hilo na kujiendeleza. Maendeleo binafsi yanasaidia kwa kiasi kikubwa kuinua maendeleo ya nchi hivyo kundi hili la watu lisivunjike moyo na kukubali kuwa hawana nafasi katika maendeleo ya nchi.

Tags: elimumaendeleoSoko la ajirauchumi
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Watumiaji wa daraja la Kigamboni kuendelea kulipa

Discussion about this post

Habari Mpya

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 27, 2022

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

by Jensen Kato
June 27, 2022
0

Kilimo biashara kinaendelea kukua barani Afrika na muda umefika kwa watu hususani vijana kuchagamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo. Watu...

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In