• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Umuhimu wa urithi, mirathi na wosia

Patricia Richard by Patricia Richard
June 26, 2018
in HABARI ZA AFRIKA MASHARIKI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Hapa Tanzania, asilimia kubwa ya watu hawana ufahamu au uelewa kuhusu masuala ya mirathi na kuandika wosia kabla ya umauti. Suala hili limekuwa geni katika jamii yetu na ni wachache sana wanaofahamu umuhimu wa haya. Wadau wa sheria, haki za binadamu pamoja na mashirika mengine husika wamekuwa hawaweki mkazo katika suala hili kama ilivyo kwa mengine. Lakini bila shaka tumeshuhudia wajane, watoto na ndugu waliofiwa na mpendwa wao wakiteseka mahakamani ili kupata haki zao na kuendesha maisha yao kama ilivyokuwa awali.

Ni wazi kuwa walio wengi wanakosa elimu ya mambo haya jambo ambalo linapelekea migogoro ya kifamilia. Unakuta ndugu wanatumia muda na fedha nyingi mahakamani pale inapotokea wamempoteza mtu ambaye hakubahatika kuandaa wosia hivyo kila mtu anataka mali fulani ili maisha yake yaendelee na asiyumbe kiuchumi. Inawezekana fedha hizi na muda wanaotumia kutafuta haki zao zingeweza kuwekezwa katika harakati nyingine za kimaendeleo na kuwaletea faida.

Jifikirie kama itatokea kesho haupo tena duniani familia yako unaiacha vipi? Wataendelea kuishi katika nyumba yao? Watoto wataendelea na masomo yao? Biashara nazo zitaenda? Kiufupi ni lazima tujiulize mara mbili kuwa hawa utakao waacha nyuma unawaacha vipi? Katika nchi zilizoendelea watu wengi wana uelewa wa mambo ya mirathi na hivyo wengi hujiandaa mapema ili kujihakikishia kuwa hata wasipokuwepo, waliopo hawataachwa katika hali ya sintofahamu.

ADVERTISEMENT

Hali hapa kwetu ni tofauti. Wengine wanaamini kuwa kuandaa wosia ni kujitakia mabaya, wengine hawaruhusiwi kufanya hivyo kutokana na itikadi za dini au kabila. Mbali na changamoto hizo, ni wazi kuwa elimu haijatolewa vya kutosha katika jambo hili. Tatizo la migogoro katika familia baada ya misiba limekuwa kubwa sana hapa kwetu na kwa kiasi kikubwa linaathiri shughuli nyingine za maendeleo. Watu wanashindwa kuendelea mbele kutokana na kwamba hawajui haki zao, wamekosa elimu stahiki la urithi na pia wanakosa usaidizi wa kisheria kutatua matatizo kama haya.

Migogoro hii imekuwa ikiwazuia wengi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi hivyo ni lazima suala hii litafutiwe suluhisho. Ni lazima jamii ielimishwe na wataalamu wa sheria kuhusu mirathi na haki zao za msingi. Ni lazima tujenge mazoea ya kufuatilia masuala kama haya kwani mara nyingi yanakuwa na madhara makubwa huko mbele.

Wakati wa kuachana na imani potofu ya kuwa kuandika wosia ni kujitabiria kifo umefika. Ni muhimu kwa jamii kujenga utaratibu wa kutayarisha wosia ili kuepusha migogoro ya aina yoyote katika familia. Elimu zaidi iendelee kutolewa ili kuwafahamisha watanzania kuhusu umuhimu wa kuandaa wosia.

Tags: elimuFamiliafedhaWosia
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Dk.Mpango kuwaneemesha wafugaji

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In