• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Unafahamu soko lako vizuri?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in BIASHARA NDOGO NDOGO
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kama mojawapo ya harakati za kujiongeza na kutengeneza kipato, watu wengi zaidi wamekuwa wakijiajiri kupitia biashara ndogo ndogo. Japokuwa wengi wamekuwa wakiona mafanikio na kutoa ushuhuda kuwa biashara inalipa, wengine hawakupata bahati hiyo na kujikuta wakipata hasara na kuwa katika hali mbaya kiuchumi. Ni kweli kupitia sekta hii, wengine wameweza kujiajiri na hata kufikia hatua ya kuajiri wengine. Vilevile, serikali nayo inafaidika na biashara hizi kupitia ukusanyaji wa mapato. Hii inamaanisha kuwa, biashara ni nguzo moja muhimu katika kuleta maendeleo hapa nchini. Lakini swali la msingi hapa ni, unafahamu vizuri soko lako?

Ni vizuri kujiuliza swali hili kama unafikiria kufanya biashara. Hata wale ambao tayari ni wafanyabiashara lakini wanataka kufika mbali zaidi kupitia hicho wanachofanya. Msingi wa biashara yoyote ile ni soko kwani hakuna biashara ambayo itafanikiwa pasipo kupokelewa vizuri na watu. Hivyo swali hili linabeba uzito mkubwa na mfanyabiashara anapaswa kujipanga na kuhakikisha kuwa anafahamu anaowalenga mwanzoni kabisa mwa mipango yake. Kama mfanyabiashara unamuuzia nani? Unalenga kundi fulani maalum kuwa wateja wako wakubwa?

ADVERTISEMENT

Ukitafakari hayo ni vizuri kuwa na mipangilio madhubuti ambayo itakusaidia kwa kiasi kikubwa kufikia malengo uliyojiwekea. Mfano umedhamiria kufanya wanafunzi wa vyuo kuwa wateja wako, utafanyaje kuhakikisha bidhaa zako zinawafikia kwa urahisi? Utakabiliana vipi na ushindani? Utakuwa unauza kwa bei iliyo rafiki kwao?

Ili kuona biashara yako inafika mbali na kukuletea faida ni vizuri kama ukafahamu vizuri unawalenga wakina nani haswa. Kufahamu soko lako kunasaidia kujua ni namna gani ya kutangaza bidhaa zako, namna gani bidhaa zako zitawafikia watu wengi na vilevile vinampa wepesi mfanyabiashara kuwa makini na kuelewa nini wateja wake wanahitaji bila ya kuingia hasara tofauti na yule ambae hana soko maalum hivyo anatumia muda mrefu zaidi kujitangaza, kujenga uaminifu na kuwavutia wateja. Kufahamu ni aina gani ya watu huvutiwa na kununua bidhaa zako zaidi humsaidia mfanyabiashara kufahamu ni wapi haswa anatakiwa kuwekeza fedha zake ili uwekezaji wake umfaidishe baadae.

Baada ya kufahamu soko lako, biashara yako ina nafasi kubwa ya kukua kama utatumia mbinu bora zaidi kujitangaza ili kuwafikia watu wengi zaidi. Mfano kama unawalenga wanafunzi wa chuo, unaweza kujitangaza kwa kiasi kikubwa kupitia mitandao ya kijamii. Matumizi ya mitandao hii yamerahisisha biashara kwa kiasi kikubwa hivyo mfanyabiashara akitumia mitandao vizuri, anaweza kuwafikia watu wengi zaidi kwa kutumia gharama ndogo na muda mfupi.

Sekta hii ni muhimu katika maendeleo ya nchi yoyote na hivyo kuna ushindani mkubwa kuhakikisha kila mfanyabiashara anavutia wateja kuja kwake. Kuelewa soko inasaidia kwa kiasi kikubwa kukuweka katika nafasi nzuri kibiashara. Wafanyabiashara wanatakiwa kufanya utafiti ili kubaini wakina nani haswa ni soko lao na ni nini wanahitaji kutoka kwako.

 

 

Tags: biasharafedhasokouwekezajiwateja
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Iache pesa yako ikutumikie

Discussion about this post

Habari Mpya

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amewasihi mashabiki wa Simba wamtie nguvu Mwekezaji Mohammed Dewji (Mo Dewji) kwa...

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Rais Samia amesema Serikali imetenga hadi eka 10 kwa kila kijana mwenye sifa za kufanya kilimo nchini Tanzania ili kuiwezesha...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In